Wizara ya Maji imejizatiti katika kukomesha changamoto ya upotevu wa maji kwa lengo la kuboresha huduma ya majisafi na salama kwa wananchi.
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amesema changamoto hiyo ni vita inayotokana na sababu mbalimbali za kiufundi na za kibiashara na kusabisha upotevu wa mapato na kuzorotesha huduma.
Amesisitiza kuwa hatamvumilia mtumishi yoyote atakayeshindwa kumaliza changamoto hiyo aidha kwa kukosa uaminifu au kwa uzembe.




