Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani linamshikilia Ally Shabani (29), mganga wa tiba asili na mkazi wa Makazi Mapya, Mlandizi wilayani Kibaha, kwa tuhuma za mauaji ya Juma Nyambihira.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Muhudhwari Msuya, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), alisema tukio hilo lilifichuka baada ya ndugu wa marehemu kutoa taarifa ya kupotea kwake tangu Agosti 17. Taarifa hizo zilikabidhiwa Kituo cha Polisi Mlandizi mnamo Agosti 29, mwaka huu.
Kwa mujibu wa ACP Msuya, baada ya taarifa hizo polisi walifungua jalada la uchunguzi na kuanza kufuatilia. Hatua hiyo ilimfikisha mikononi mwao mtuhumiwa Shabani, ambaye inadaiwa alikuwa akiishi na marehemu Juma akimpatia matibabu ya asili kutokana na tatizo la uoni hafifu.
Mwili Wapatikana Katika Shimo
Kamanda Msuya alieleza kuwa mnamo Septemba 3, wakati upelelezi ukiendelea, askari walifika nyumbani alipokuwa akiishi mtuhumiwa pamoja na marehemu kwa ajili ya upekuzi. Katika eneo hilo, walibaini uwepo wa tanuri la mkaa lililokuwa karibu na nyumba hiyo, ambapo kando yake kulionekana dalili za shimo.
“Baada ya kufukuliwa, tulibaini ndani ya shimo hilo ulikuwa mwili wa marehemu Juma Nyambihira,” alisema ACP Msuya.
Mwili wa marehemu unatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.
Mtuhumiwa Kufikishwa Mahakamani
Jeshi la Polisi limeeleza kuwa mtuhumiwa Ally Shabani atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika, huku likiendelea na hatua za uchunguzi ili kubaini undani wa tukio hilo.
The 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee concluded in BEXCO, Busan, Republic of Korea, on July 29, 2026. The historic 10-day meeting approved 28 total property actions, adding 25 new sites to the World Heritage List and bringing total World Heritage properties to 1,273. Delegates from 196 States Parties to the World Heritage Convention of the United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) and UNESCO’s advisory bodies ICOMOS and IUCN are attending the 48th session of the UNESCO World Heritage Committee (WHC).
Approximately 3,000 delegates, including the Director-General of UNESCO, representatives from Member States, Ministerial-level officials and Deputy Ministers from 21 member states that constitutes the World Heritage Committee attended the session.
The Permanent Mission of Tanzania to UNESCO in collaboration with the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania organized a side event to brief UNESCO Member States from around the world on the findings of the two Presidential Commissions that conducted an assessment of land issues and voluntary relocation from the Ngorongoro Conservation Area.
The reporter also received further clarification from Prof. Hamisi Malebo, Executive Secretary of the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania, that the side event is an effort by the Government to respond to calls that have been made by various United Nations Experts, UNESCO advisory bodies and organizations requesting the Government to publish the results and full report of the Presidential Commissions that conducted an assessment of land issues and voluntary relocation from the Ngorongoro Conservation Area.
Contributing to the discussion during the Ngorongoro Side Event at the 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee, Mr. Isack Lekisongo Meijo, a Maasai Traditional Leader from Tanzania, underscored the historic relationship between the Maasai people, livestock and wildlife within the Ngorongoro Conservation Area (NCA). Mr. Meijo emphasized that traditional Maasai pastoralism has, for generations, coexisted with wildlife though with difficulties attributable to human wildlife interactions, but have contributed to the conservation of the Ngorongoro ecosystem.
He said, “there is no Ngorongoro without the Maasai pastoralists, and there is no Ngorongoro without the wildlife.” Using a powerful metaphor to illustrate the challenge of balancing conservation and human development, he stated: “Ngorongoro is like an aircraft carrying pastoralists, livestock and wildlife. Today, the aircraft is fully loaded, indeed overloaded. If it attempts to take off carrying more than its safe capacity, it risks crashing. For a safe and sustainable journey, it must offload its excess luggage in a carefully planned and balanced manner.”
Mr. Meijo explained that the metaphor reflects the growing pressures on the finite ecosystem of the Ngorongoro Conservation Area, where increasing human populations, human settlements, livestock and wildlife coexist within the same landscape which is not expanding under the Multiple Land Use Model (MLUM). He observed that the international discussion on achieving an appropriate balance between conservation and sustainable human development has generated differing perspectives.
One school of thought advocates reducing pressure on the ecosystem through the voluntary relocation of pastoralist households and their livestock to areas with expanded social and economic opportunities. Another perspective argues for relocating wildlife to other areas beyond the Conservation Area to reduce ecological pressure. The MLUM in the NCA faces severe sustainability strains as growing human populations, livestock, and wildlife share a fixed land size which at the moment it has taken a collapsing gravity, and this is a wake-up call to rescue Ngorongoro.
Mr. Meijo stressed that, regardless of differing views, the common objective is to safeguard the Outstanding Universal Value of the Ngorongoro Conservation Area while ensuring sustainable livelihoods for present and future generations of the Maasai community. He concluded by reaffirming the commitment of the Maasai community to continue working with the Government of Tanzania, UNESCO, IUCN, ICOMOS and all stakeholders to ensure that Ngorongoro remains a globally significant World Heritage Site where conservation, culture and sustainable development reinforce one another.
Following immediately after Mr. Meijo’s call, a delegate from Zimbabwe questioned and wanted to know at the operation level between the two, which option carries more risks between the relocation of pastoralists and their livestock or relocating wildlife from Ngorongoro Conservation area to reduce ecological pressure? Responding to the question on behalf of the Government of the United Republic of Tanzania, Prof. Hamisi Malebo, the Executive Secretary of the UNESCO National Commission of Tanzania, told the meeting that the easiest option is to educate and request for voluntary relocation and that can only be done with humans.
Prof. Malebo told the meeting further that, relocating wild animals is far more complex and dangerous than moving human populations, involving immense logistical hurdles, severe financial costs, and the permanent disruption of ancient, finely-tuned natural phenomena, the seasonal movement of over 1.5 million wildebeest. He reiterated the position of the Government of the United Republic of Tanzania which on the same reasons is relocating Maasai pastoralists outside of the Ngorongoro Conservation Area.
Delegates and representatives from 36 countries expressed gratitude to the Government of the United Republic of Tanzania for hosting an informative side event on the Ngorongoro Conservation Area during the 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee in Busan, South Korea. Contributions from the majority of the delegates conceded that, maintaining balance in the Ngorongoro Conservation Area is complex due to soaring human populations, wide spreading human settlements, rising livestock numbers, and shrinking wildlife grazing space and corridor.
The mixed land-use model is unsustainable due to severe pressure from overgrazing, human-wildlife conflicts, and climate change. The event brought together Permanent Delegates to UNESCO, International Ambassadors, Members of the World Heritage Committee, Maasai Traditional Leaders, Conservation Experts, The Pastoralists Indigenous Non-Governmental Organizations Forum (PINGOs Forum), the Maasai International Solidarity Alliance (MISA) and other stakeholders to discuss the future of the Ngorongoro Conservation Area.
On his opening remarks Ambassador His Excellence Saidi Yakubu, The Permanent Representative of Tanzania to UNESCO and Ambassador of Tanzania to France, stressed that sustainable conservation requires openness, honest talks, and teamwork. The session highlighted collaborative efforts with UNESCO and the IUCN to align ecological preservation with the welfare of local communities.
Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeshiriki Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma mwaka 2026 linaloendelea jijini Arusha, limewakutanisha wadau wa ununuzi pamoja na viongozi wa Serikali kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuimarisha Sekta ya ununuzi na ugavi nchini.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando, Mkuu wa Sehemu ya Huduma za Sheria PPAA, Agnes Sayi amewahimiza wadau wa ununuzi wa umma kutembelea banda la Mamlaka ya Rufani kupata uelewa juu ya majukumu na huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo hususan matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST.
PPAA imeshiriki maonesho yanayofanyika pembezoni mwa Kongamano hilo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na mchakato wa ununuzi wa umma, uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na kufungiwa kushiriki katika michakato ya ununuzi wa umma pamoja na uamuzi juu ya malalamiko yanayotokana na kushindwa kwa Afisa Masuuli kutoa uamuzi ndani ya muda uliowekwa.
Awali, akifungua Kongamano hilo kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dk. Toba Nguvila amesema sekta ya ununuzi wa umma inahusisha sehemu kubwa ya matumizi ya fedha za serikali, hivyo kuna ulazima wa kuhakikisha fedha zote zinazotengwa zinasimamiwa kwa umakini mkubwa ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa.
Dk. Nguvila amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika mfumo wa ununuzi wa umma ili kuongeza uwazi, kupunguza gharama za ununuzi, kuharakisha mchakato na kurahisisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma.
“Ununuzi wa umma na ugavi ni nyenzo ya kisera na kimkakati ya Serikali katika kuchochea uzalishaji, ukuaji wa viwanda, kuongeza ajira, kuimarisha kampuni za ndani, kukuza ubunifu, na kuhakikisha maendeleo yanayopatikana yanawanufaisha Watanzania wengi zaidi,” amesema Dk. Nguvila.
Kongamano hilo la siku tatu limeanza tarehe 29 – 31 Julai, 2026 limewakutanisha wadau wa ununuzi zaidi ya 1,500. Aidha, limewakutanisha Wakuu wa Taasisi, Maafisa Masuuli, Maafisa Ununuzi, Idara Tumizi, Maafisa Sheria, Wazabuni na Taasisi binafsi.
📌Experts say the river’s future depends on stronger scientific research, regional cooperation and cultural preservation.
Addis Ababa, 30 July 2026 – Calls for deeper scientific collaboration, stronger regional partnerships, and greater investment in preserving one of Africa’s most important waterways dominated discussions on the opening day of the World Public Summit in Addis Ababa, Ethiopia.
Researchers and cultural experts unveiled an ambitious international study on the Zambezi River, emphasising that its future hinges on robust scientific research, regional cooperation, and cultural preservation.
During a roundtable titled “Zambezi River: Economy, Society, Soul,” participants described the initiative as more than a research project, saying it is designed to generate practical solutions that will improve livelihoods, protect ecosystems, and preserve the shared cultural heritage of communities living along the river.
The interdisciplinary study will examine the socioeconomic impact of the Zambezi River across Angola, Zambia, Zimbabwe, Namibia, Botswana, and Mozambique, while also considering the wider river basin, including Tanzania and Malawi. The project aligns with the African Union’s 2026 theme, “Ensuring Sustainable Access to Water and Safe Sanitation to Achieve the Goals of Agenda 2063.”
Ivan Zakharov, a researcher at the Institute for African Studies of the Russian Academy of Sciences, highlighted the Zambezi as a unique opportunity to demonstrate how transboundary water resources could be studied and managed through international cooperation. “I think it has a bright future,” Zakharov said, adding that the project could become “a very interesting role model” for other river basins, including the Nile.
He explained that researchers intend to undertake extensive field studies covering economics, international relations, history, social geography, and anthropology. The comprehensive approach will help to better understand how communities interact with the river, given its very diverse climatic and hydrological properties.
“We need to engage all the countries in this river basin to understand migration patterns during the dry season, the rainy season, and especially when floods are coming. This will allow us to trace these patterns and try to eliminate negative consequences such as conflicts,” Zakharov emphasised. He noted that such research could help reduce disputes and support more coordinated development policies among countries sharing the river.
For Zambia’s National Livingstone Museum Director and cultural historian Victoria Phiri Chitungu, the summit transformed what began as an informal idea into a structured international initiative backed by scientific institutions.
“I came here with the idea of the Zambezi River project, which was just an idea among friends. But coming to this conference, it has put it into a conceptualised idea, like a tangible project,” she said.
Chitungu noted that discussions had broadened the project’s scope beyond documenting the river’s six mainstream countries to considering the entire basin and the interconnected communities whose livelihoods depend on it.
She added that researchers hope to document the cultures, languages, traditions, wildlife, and ecosystems found along the river, while exploring how changing economies, population growth, and climate change are reshaping the region.
“If we don’t study the river, if we don’t appreciate it, if we don’t know what’s happening around it, it means that this river might not be preserved,” she warned, noting that several African rivers have already disappeared due to environmental degradation.
Beyond scientific research, the project also seeks to create educational and cultural spaces that make knowledge about the Zambezi accessible to students, researchers, and the wider public.
Russian student Svetlana Dubeykovskaya presented architectural concepts developed by young Russian designers for a cultural complex in Zambia’s Lower Zambezi region. She explained that these proposals demonstrated how architecture could support education and community development.
“People spent six months on these projects. They thought about every single thing and researched a lot about the region,” she said.
She expressed hope that architects from Africa and Russia would eventually work together to transform the concepts into practical projects capable of improving people’s lives while celebrating the region’s cultural identity.
Yanina Dubeykovskaya, Deputy Executive Director of the World Peoples Assembly and President of the Association of Women Public Figures “Women’s Influence,” affirmed that the Addis Ababa discussions marked only the beginning of a long-term international partnership.
“We are not only meeting each other once in three years, but we are doing common projects,” she said.
She announced that participating institutions would continue refining the initiative ahead of presentations planned during the Russia-Africa track in Moscow later this year, where researchers hope to unveil exhibition concepts and a common scientific methodology for the study.
According to the project framework, museums and universities from Russia, Angola, Zambia, Zimbabwe, Namibia, Botswana, and Mozambique will collaborate on research expeditions throughout 2027. This will culminate in a comprehensive scientific report, policy recommendations, exhibitions, photographic archives, and educational materials.
Participants said the initiative represents a new model of Africa-centred international research, bringing together science, culture, and development planning to ensure that the Zambezi River remains both a source of economic opportunity and a shared natural and cultural heritage for future generations.
Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) kimetangaza kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa kielektroniki wa kurahisisha shughuli za uingizaji na usafirishaji wa bidhaa kuanzia Agosti 1, 2026.
Mfumo huo umeunganishwa na Tanzania Electronic Single Window (TANESW) kwa lengo la kuongeza ufanisi, uwazi na kurahisisha utoaji wa huduma za uwakala wa forodha kwa njia ya kielektroniki. TAFFA imesema mfumo huo utatumika katika uingizaji wa bidhaa nchini, usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi pamoja na mizigo ya transit inayopita Tanzania Bara kuelekea nchi jirani, isipokuwa bidhaa au huduma zilizosamehewa chini ya GN Na. 83 ya mwaka 2026. Utekelezaji utaanza kwa awamu ya majaribio kwa kushirikisha baadhi ya kampuni za uwakala wa forodha kabla ya mfumo huo kuanza kutumika rasmi kwa wadau wote. TAFFA imewataka wanachama na wadau wa biashara kujiandaa mapema kwa matumizi ya mfumo huo na kufuatilia taarifa rasmi kuhusu usajili, mafunzo na taratibu za matumizi kupitia njia rasmi za chama.
Global Education Link (GEL) imesema jumla ya wanafunzi, wazazi na walezi 1,113 wamefikiwa na kupatiwa huduma kupitia maonesho ya Global Education Fair 2026 yaliyofanyika Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam na tarehe 30 maonesho kama hayo yatafanyika Rockcity Mall Mwanza.
Akizungumza baada ya kukamilika kwa maonesho yaliyofanyika Julai 25, 2026 katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa GEL, Abdulmalik Mollel, alisema mwitikio huo unaonesha kuongezeka kwa uhitaji wa taarifa sahihi kuhusu fursa za kusoma nje ya nchi.
Alisema kupitia maonesho hayo, washiriki walipata ushauri kuhusu uchaguzi wa kozi, vyuo vikuu, scholarships, gharama za masomo, malazi, visa na maisha ya mwanafunzi katika mataifa mbalimbali.
“Mwitikio tulioupata Zanzibar, Dodoma na Dar es Salaam unaonesha kuwa wanafunzi na wazazi wanahitaji mwongozo sahihi kabla ya kufanya maamuzi kuhusu elimu ya juu,” alisema Bwana Mollel.
Alisema zaidi ya watu 700 walitembelea banda la GEL katika maonesho yaliyofanyika Viwanja vya Maisara, Zanzibar, watu 168 walihudhuria maonesho ya Dodoma na wengine 245 walishiriki maonesho ya Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mollel, jumla ya maombi 209 ya udahili yaliwasilishwa kupitia maonesho hayo matatu.
Alisema Zanzibar ilipokea maombi 79 ya udahili katika vyuo vikuu vya China, India, Malaysia, Afrika Kusini na mataifa mengine, ambapo wanafunzi 30 walipata udahili papo kwa papo.
Kwa upande wa Dodoma, maombi 78 yaliwasilishwa, wanafunzi 50 wakapata udahili papo kwa hapo na wengine 40 wakafungua mafaili mapya kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kujiunga na vyuo.
Katika maonesho ya Dar es Salaam, watu 108 walionesha nia ya kuendelea na taratibu za udahili, maombi 52 yaliwasilishwa, barua 41 za udahili zilikuwa tayari na mafaili mapya 15 yalifunguliwa.
Alisema mafanikio hayo yametokana na kuwapa wanafunzi nafasi ya kukutana moja kwa moja na wawakilishi wa vyuo vikuu, kuuliza maswali na kupata ushauri unaozingatia matokeo yao ya kitaaluma, uwezo wa kifedha na malengo ya baadaye.
Mollel alisema Global Education Fair hailengi kuwasaidia wanafunzi kupata udahili pekee, bali pia kuwajengea uwezo wa kuchagua taaluma zenye fursa katika soko la ajira na zinazoweza kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.
“Tunataka mwanafunzi achague kozi inayolingana na uwezo wake, mahitaji ya soko la ajira na mchango anaoweza kuutoa katika maendeleo ya Taifa, badala ya kuchagua kwa kufuata mkumbo,” alisema.
Alitaja baadhi ya maeneo yenye fursa kuwa ni sayansi za afya na tiba, uhandisi, teknolojia ya habari na mawasiliano, akili bandia, sayansi ya data, usalama wa mtandao, nishati, kilimo cha kisasa, biashara, fedha, usafirishaji, utalii, elimu na teknolojia za viwanda.
Katika maonesho ya Dar es Salaam, vyuo vilivyoshiriki ni pamoja na Lovely Professional University, Sharda University, SRM University–AP, Maharishi Markandeshwar (Deemed to be University)—MMU, Noida International University na Asia Pacific University of Technology and Innovation.
Pia kulikuwa na mabanda yaliyotoa taarifa kuhusu fursa za kusoma China, Malaysia, North Cyprus, Marekani, Canada, Uingereza, Uholanzi, Australia, Ireland, New Zealand na Dubai.
Mollel aliwaalika wakazi wa Kanda ya Kaskazini kushiriki maonesho yatakayofanyika Julai 28, 2026 katika Hoteli ya Four Points by Sheraton jijini Arusha.
Aidha, aliwaalika wakazi wa Kanda ya Ziwa kufika kwenye maonesho yatakayofanyika Julai 30, 2026 katika Rock City Mall jijini Mwanza, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni.
Aliwataka wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne, Kidato cha Sita, stashahada, shahada na wale wanaotafuta nafasi za masomo ya uzamili kufika wakiwa na matokeo au vyeti vyao.
“Tunawaalika wanafunzi, wazazi na walezi wa Arusha, Mwanza na mikoa ya jirani kufika na kupata ushauri wa moja kwa moja kuhusu kozi, vyuo, udahili na scholarships,” alisema Mollel.
Alisema GEL itaendelea kuwaongoza wanafunzi kuanzia hatua ya kuchagua kozi na chuo, kuomba udahili, kupata visa na malazi hadi maandalizi ya safari ya kwenda kusoma nje ya nchi.
Kituo cha Kimataifa cha Dini na Utamaduni (SCJTV) kimesema wasiwasi unaongezeka kuhusu ubaguzi na unyanyapaa dhidi ya wanachama wa Shincheonji Kanisa la Yesu, Hema la Hekalu la Ushuhuda, waliopo nje ya Korea Kusini.
Taarifa hiyo imekuja baada ya shirika la kimataifa la haki za binadamu, *Coordination des Associations et Particuliers pour la Liberté de Conscience (CAP LC), kuwasilisha taarifa ya pamoja ya maandishi katika *Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, likisisitiza umuhimu wa kuhakikisha maamuzi ya kiutawala na kimahakama yanazingatia ushahidi unaoweza kuthibitishwa na viwango vya wazi vya kisheria.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Julai 9, 2026, CAP LC iliwasilisha taarifa hiyo kwa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa pamoja na shirika lisilo la kiserikali la United for Human Rights, likieleza wasiwasi kuhusu kuenea kwa ubaguzi na unyanyapaa dhidi ya wanachama wa Shincheonji Kanisa la Yesu.
Taarifa hiyo iliwasilishwa katika Kikao cha 62 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, kilichofanyika Juni 15 hadi Julai 10, 2026, chini ya Ajenda Na. 3 inayohusu kukuza na kulinda haki zote za binadamu, ikiwemo haki za kiraia, kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni pamoja na haki ya maendeleo.
Katika taarifa yake, CAP LC ilijikita zaidi katika viwango vinavyopaswa kutumika kutathmini masuala ya haki za binadamu kuliko mabishano yanayohusu Shincheonji Kanisa la Yesu yenyewe.
Shirika hilo lilieleza wasiwasi kwamba mitazamo hasi na taarifa ambazo hazijathibitishwa, zikiwemo taarifa zinazotengenezwa nchini Korea Kusini na kusambazwa katika nchi nyingine, zinaweza kuwa na athari kubwa kwa maoni ya umma pamoja na maamuzi ya kiutawala na kimahakama.
Kwa msingi huo, CAP LC imezitaka serikali kuhakikisha kuwa maamuzi yoyote yanayohusu Shincheonji Kanisa la Yesu yanategemea ushahidi unaoweza kuthibitishwa na viwango vya wazi vya kisheria.
Shincheonji Kanisa la Yesu limesema hatua hiyo inaonyesha umuhimu wa kulinda haki za makundi ya kidini yaliyo wachache, likisema kuwa endapo unyanyapaa usio na msingi utaruhusiwa kukubalika kimataifa, makundi mengine ya kidini yaliyo wachache yanaweza pia kukabiliwa na hukumu na ubaguzi wa aina hiyo.
Kwa mujibu wa kanisa hilo, hali hiyo inaonyesha wajibu wa mataifa kuhakikisha kuwa haki za makundi yote ya kidini yaliyo wachache zinalindwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
CAP LC, ambalo lina hadhi maalum ya ushauri katika Baraza la Uchumi na Masuala ya Kijamii la Umoja wa Mataifa (ECOSOC), ni shirika la kimataifa lisilo la kiserikali linalojihusisha kwa muda mrefu na masuala ya uhuru wa dini katika ngazi ya kimataifa.
Hapo awali, CAP LC limewasilisha mbele ya Umoja wa Mataifa masuala yanayohusu mateso dhidi ya Church of Almighty God nchini China, pamoja na wasiwasi kuhusu ukiukwaji wa uhuru wa dini uliotokana na ombi la Serikali ya Japan la kutaka kutolewa kwa amri ya kuvunjwa kwa taasisi inayojulikana rasmi kama *Family Federation for World Peace and Unification, ambayo awali ilifahamika kama *Unification Church.
Shincheonji Kanisa la Yesu limesema ukweli kwamba shirika la kimataifa lisilo la kiserikali limewasilisha taarifa kuhusu suala hilo unaonyesha kuwa kesi inayolihusu kanisa hilo si jambo la ndani la Korea Kusini pekee, bali pia imeanza kuvutia uangalizi wa kimataifa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
Unyanyapaa Bila Ushahidi
Taarifa hiyo pia imetaja mifano kutoka Uingereza na nchi zinazozungumza Kijerumani, ikisema mitazamo hasi dhidi ya wanachama wa Shincheonji Kanisa la Yesu imevuka mipaka ya maoni ya umma na kusababisha taratibu za kiutawala pamoja na kuingiliwa kwa maisha ya kijamii ya baadhi ya watu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mifano hiyo inaonyesha namna unyanyapaa usio na ushahidi wa kutosha unavyoweza kugeuka kuwa ubaguzi wa kijamii na hatimaye kuathiri haki na maisha ya watu binafsi.
CAP LC imesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa hatua za serikali na taasisi za mahakama dhidi ya makundi ya kidini zinachukuliwa kwa kuzingatia ushahidi unaoweza kuthibitishwa, taratibu za haki na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu.
📌 Kazi za uvutaji waya kwenye mradi kusababisha katizo la muda la umeme katika baadhi ya maeneo kwa ratiba maalumu
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Msongo wa Kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Dodoma uko kwenye hatua za mwisho za utekelezaji wake, huku ujenzi ukiwa umekamilika kwa asilimia 94 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 21, 2026.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 28, 2026, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa TANESCO, Irene Gowelle, amesema ili kuwezesha ukamilishaji wa kazi za mradi huo kutakuwepo na katizo la muda la umeme katika baadhi ya maeneo nchini kwa ratiba maalumu kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itakua Julai 30 hadi Agosti 4 na ya pili itaanza Agosti 11 hadi 17, 2026.
Gowelle amesema hatua hiyo ni sehemu ya maandalizi ya ombi la Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kampuni ya TBEA ambayo inalenga kuhakikisha kazi zinafanyika kwa hali ya usalama .
“Mradi huu umefikia hatua muhimu sana ya utekelezaji ambapo kipindi hiki, baadhi ya njia za kusafirisha umeme za kilovolti 220 na 132 zitalazimika kuzimwa kwa muda ili kuruhusu kazi za kuvuta na kuunganisha nyaya mpya kufanyika kwa usalama. Hii ni hatua ya kawaida katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu ya kusafirisha umeme na inalenga kukamilisha mradi huu wenye manufaa makubwa kwa Taifa,” amesema Gowelle.
Amefafanua kuwa baadhi ya maeneo katika mikoa iliyoko Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa, Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Magharibi na Kanda ya Kusini Magharibi inaweza kuathiriwa kwa nyakati tofauti kulingana na ratiba za utekelezaji wa kazi hizo.
Gowelle amesema TANESCO itaendelea kutoa taarifa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na majukwaa mbalimbali ya mawasiliano ili kuwawezesha wateja kupanga matumizi yao ya umeme kwa kuzingatia ratiba zitakazotolewa.
Aidha, amesisitiza kuwa Tanzania ina umeme wa kutosha na kwamba katizo hilo ni la muda, likiwa ni sehemu ya kukamilisha mradi huo wa kimkakati unaolenga kuimarisha uwezo wa usafirishaji wa umeme nchini. Ameongeza kuwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara haitahusika katika ratiba hiyo ya katizo.
Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme ya Kilovolti 400 Chalinze–Dodoma, Mhandisi Newton Mwakifwamba, amesema mradi huo wenye urefu wa kilomita 345 na thamani ya takribani shilingi bilioni 514 umefadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema mradi unahusisha ujenzi wa njia mpya ya kusafirisha umeme pamoja na upanuzi wa vituo vya kupokea na kusambaza umeme vya Chalinze na Dodoma.
“Katika hatua hizi za mwisho, tutafanya kazi za kuvusha na kuunganisha njia mpya ya umeme katika maeneo ya Mkambarani, Kikombo na Mkonze. Hatua hizi ni muhimu ili kuhakikisha mradi unaanza kufanya kazi kwa ufanisi na usalama,” amesema Mhandisi Mwakifwamba.
Ameongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaimarisha uwezo wa mfumo wa taifa wa usafirishaji umeme na kuwezesha usafirishaji wa umeme unaozalishwa katika Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere kwenda maeneo mbalimbali ya nchi, hatua itakayoimarisha uhakika wa upatikanaji wa umeme na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Fadhili Maganya, amepongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa utekelezaji mzuri wa mpango wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.
Maganya amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa na Manispaa hiyo, akisema imepiga hatua kubwa katika utoaji wa mikopo na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikilinganishwa na maeneo mengine nchini.
Amesema hayo Julai 27, 2026 katika mkutano wa ndani wa chama uliofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, baada ya kumuhoji Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dk. Rogers Shemwelekwa, kuhusu utekelezaji wa mikopo hiyo.
“CCM tunataka utekelezaji wa Ilani kwa vitendo, na hapa tumeona kazi inayofanyika yenye manufaa kwa Serikali na wananchi wa Manispaa ya Kibaha,” amesema Maganya.
Kwa upande wake, Dk. Shemwelekwa amesema Manispaa ya Kibaha hadi sasa imetoa zaidi ya Sh bilioni 2.1 kwa vikundi 400, huku wanufaika zaidi ya 3,000 wakinufaika na mikopo hiyo.
Amesema Manispaa hiyo inaendelea na maandalizi ya kutoa mikopo mingine katika mwaka wa fedha 2026/2027 ili kuwafikia wajasiriamali wengi zaidi.
Ameeleza kuwa kabla ya utoaji wa mikopo hiyo, alifanya ziara katika mitaa na kata mbalimbali kutoa elimu kwa wananchi kuhusu taratibu na vigezo vya kupata mikopo, hatua iliyosaidia kuongeza idadi ya waombaji na kuboresha marejesho.
Maganya amesema hatua hiyo ni mfano wa utekelezaji unaopaswa kuigwa na halmashauri nyingine nchini, huku akimtaka Mkurugenzi kuhakikisha wataalamu wanawafikia wananchi kutoa elimu zaidi ili kuondoa vikwazo vinavyowafanya baadhi kushindwa kufikia sifa za kupata mikopo.
Mbunge wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kuifanya Kibaha kuwa Manispaa, akisema hatua hiyo imechochea ukuaji wa maendeleo na kuongeza mapato ya eneo hilo.
Tanzania is accelerating efforts to position itself as a regional healthcare manufacturing hub as the government expands local pharmaceutical production, medical device manufacturing and domestic health commodity supply chains.
The drive is aimed at reducing the country’s reliance on imported medicines and healthcare products while attracting investment into the sector. The growing manufacturing capacity is also helping reshape healthcare trade across East Africa by creating opportunities for regional partnerships and market expansion.
The development comes amid a broader shift across East Africa, where governments are strengthening healthcare systems, building more resilient supply chains and promoting regional cooperation.
Tanzania’s expanding manufacturing capabilities complement Kenya’s established role as a logistics and distribution gateway, creating a more interconnected healthcare market in which manufacturers, distributors, hospital groups and investors can reach multiple markets more efficiently.
The growing opportunities are being supported by rising demand for healthcare services and technologies across the region. East Africa’s health and wellness market was estimated at USD 16.8 billion in 2025 and is projected to reach USD 23.6 billion by 2034.
Meanwhile, the region’s hospitals market is forecast to reach USD 9.25 billion, while the pharmaceuticals market is estimated at USD 2.39 billion in 2025, highlighting the expanding commercial opportunities in healthcare delivery, procurement, diagnostics and medical technologies.
Against this backdrop, healthcare stakeholders from East Africa and beyond are expected to converge in Nairobi for the 10th edition of WHX Nairobi, formerly known as Medic East Africa, scheduled for September 16–18, 2026, at the Kenyatta International Convention Centre (KICC).
Held under the patronage of Kenya’s Ministry of Health, the exhibition is expected to bring together manufacturers, distributors, healthcare providers, procurement specialists, logistics companies and policymakers to explore new technologies, forge partnerships and support healthcare growth across Africa.
Organisers expect more than 5,500 attendees, with international participants accounting for about 40 per cent. The event is also projected to feature more than 200 exhibitors from over 30 countries, alongside a 22 per cent year-on-year increase in exhibitor participation.
The exhibition floor is expected to expand to 4,500 square metres, representing an 81 per cent increase from the previous edition. The 2025 event generated an estimated USD 84.19 million in business.
“East Africa’s healthcare sector is becoming increasingly interconnected as countries invest in local manufacturing while strengthening regional trade and distribution networks,” said Tom Coleman, Portfolio Director – Healthcare at inD.
“Tanzania’s growing focus on pharmaceutical and medical device manufacturing, together with Kenya’s established logistics infrastructure, is creating new opportunities for businesses to expand across the region,” he said.
Coleman added that stronger regional collaboration would be critical to improving access to medicines, medical technologies and healthcare services for millions of people across East Africa.
The 2026 exhibition will showcase innovations across eight key sectors, including medical devices and equipment, imaging and diagnostics, laboratory technology, orthopaedics and physiotherapy, healthcare infrastructure, IT and digital health, healthcare services, and medical consumables.
As healthcare systems across East Africa continue to evolve, the event is expected to provide a platform for advancing partnerships, technology transfer and investment while supporting the development of more resilient and interconnected healthcare systems across the region.
Dar es Salaam. Benki ya NMB imewahakikishia wafanyabiashara kuendelea kuwapatia masuluhisho ya kifedha yanayolenga mahitaji ya sekta mbalimbali za uchumi. Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki katika Jukwaa la NMB Business Executive Network 2026 lililowakutanisha zaidi ya wafanyabiashara 300 kutoka Dar es Salaam na Pwani.
Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, alisema benki hiyo imeanzisha Madawati ya Kisekta ili kutoa huduma zinazolingana na mahitaji ya sekta kama madini, ujenzi, utalii, kilimo, afya na elimu. Alisema masuluhisho hayo yanajumuisha Asset Financing, Bid Bond, Advance Payment Guarantee na Performance Guarantee.
Katika jukwaa hilo, NMB pia ilitambulisha tuzo mbili za kimataifa ilizotunukiwa mwaka huu ambazo ni Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Euromoney na Tuzo ya Benki Bora zaidi kwa Wafanyabiashara Tanzania 2026 kutoka jarida la Global Finance, zikidhihirisha kutambuliwa kwake kimataifa kwa ubora wa huduma.
Jukwaa hilo lilitoa nafasi kwa wafanyabiashara na viongozi wa NMB kujadiliana kuhusu mahitaji ya sekta binafsi na namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano unaochochea ukuaji wa biashara na uchumi wa Tanzania.