Mwenyekiti wa Chama cha Wachezaji wa Mpira wa Miguu Tanzania (SPUTANZA), Mussa Kisoki, amesema malalamiko ya wachezaji kuhusu mikataba na uhamisho yamepungua kutokana na kuongezeka kwa uelewa wa wachezaji na viongozi.

Amesema pia hatua ya TFF kuwalipa wachezaji wanaodai vilabu kupitia fedha zinazotolewa kwa klabu husika imepunguza migogoro.
Aidha, SPUTANZA imejiunga na Chama cha Wachezaji wa Dunia kinachotambuliwa na FIFA kwa kanda ya Afrika, hatua itakayosaidia kubadilishana uzoefu na kuimarisha vyama vya wachezaji.




