Tuesday, April 7, 2026
spot_img
HomeMichezoVinicius amtaja Yamal kupinga ubaguzi

Vinicius amtaja Yamal kupinga ubaguzi

Staa wa Real Madrid, Vinícius Júnior, ameendelea kuwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi, akimtaja chipukizi wa FC Barcelona, Lamine Yamal, kama sehemu ya kizazi kipya kinachoweza kuendeleza mapambano hayo.

Vinícius amesema anatamani kumuona Yamal akiendelea kupaza sauti dhidi ya ubaguzi kama ambavyo yeye amekuwa akifanya kwa muda mrefu.

“Natumaini Lamine Yamal ataendelea na hii vita dhidi ya ubaguzi kama mimi. Tuko pamoja.”

Mshambuliaji huyo wa Brazil ameeleza kuwa tatizo la ubaguzi linawaathiri zaidi watu wenye maisha magumu, hususan watu weusi maskini, ambao hukutana na changamoto kubwa zaidi kuliko hata mastaa wa soka.

“Sisi tuna fedha, lakini watu weusi maskini wanapata shida zaidi kuliko sisi, na tunapaswa kupambana na ubaguzi wote kwa pamoja.”

Aidha, Vinícius amesisitiza kuwa hajalengi kuilaumu nchi yoyote moja kwa moja, bali anaamini kuwa ubaguzi upo kila sehemu duniani.

“Sisemi Hispania, Ujerumani au Ureno ni nchi za kibaguzi, lakini wabaguzi wapo kila nchi, na tukipambana pamoja, naamini watu wengi wataacha kupitia mateso haya.”

Kauli hiyo inaendeleza mjadala mpana wa kimataifa kuhusu kupinga ubaguzi wa rangi ndani na nje ya uwanja wa michezo.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments