Home Blog

Mganga wa tiba asili akamatwa kwa tuhuma za mauaji Kibaha

0

Na Mwandishi Wetu, Pwani

Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani linamshikilia Ally Shabani (29), mganga wa tiba asili na mkazi wa Makazi Mapya, Mlandizi wilayani Kibaha, kwa tuhuma za mauaji ya Juma Nyambihira.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Muhudhwari Msuya, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), alisema tukio hilo lilifichuka baada ya ndugu wa marehemu kutoa taarifa ya kupotea kwake tangu Agosti 17. Taarifa hizo zilikabidhiwa Kituo cha Polisi Mlandizi mnamo Agosti 29, mwaka huu.

Kwa mujibu wa ACP Msuya, baada ya taarifa hizo polisi walifungua jalada la uchunguzi na kuanza kufuatilia. Hatua hiyo ilimfikisha mikononi mwao mtuhumiwa Shabani, ambaye inadaiwa alikuwa akiishi na marehemu Juma akimpatia matibabu ya asili kutokana na tatizo la uoni hafifu.

Mwili Wapatikana Katika Shimo

Kamanda Msuya alieleza kuwa mnamo Septemba 3, wakati upelelezi ukiendelea, askari walifika nyumbani alipokuwa akiishi mtuhumiwa pamoja na marehemu kwa ajili ya upekuzi. Katika eneo hilo, walibaini uwepo wa tanuri la mkaa lililokuwa karibu na nyumba hiyo, ambapo kando yake kulionekana dalili za shimo.

“Baada ya kufukuliwa, tulibaini ndani ya shimo hilo ulikuwa mwili wa marehemu Juma Nyambihira,” alisema ACP Msuya.

Mwili wa marehemu unatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.

Mtuhumiwa Kufikishwa Mahakamani

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa mtuhumiwa Ally Shabani atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika, huku likiendelea na hatua za uchunguzi ili kubaini undani wa tukio hilo.

PPAA yawaelekeza wazabuni kutumia Mfumo wa NeST

0

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imewahimiza wazabuni na wadau wa ununuzi wa umma kutumia Moduli ya Kupokea na Kushughulikia Malalamiko na Rufaa katika mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST) kuwasilisha malalamiko na rufaa zao PPAA pindi wanapoona hawakutendewa haki katika michakato ya ununuzi wa umma.

Akizungumza na waandishi wa Habari pembezoni mwa Kongamano la kumi la ununuzi wa Umma la mwaka 2026 linaloendelea Jijini Arusha kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma PPAA, Nelson Kessy amesema kuanza kwa matumizi ya Moduli hiyo kuna faida nyingi kama vile kuokoa muda na gharama.

“Faida nyingine za wazabuni na taasisi nunuzi kutumia moduli ni pamoja na kuongeza uwazi na uwajibikaji pamoja na kuwezesha utunzaji wa kumbukumbu sahihi za malalamiko na rufaa zinazowasilishwa na wazabuni, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa uamuzi,” amesema Kessy

Kessy ameongeza kuwa Mamlaka ya Rufani inawaelekeza wazabuni wote wa ndani na nje ya nchi kutumia Moduli ya kuwasilisha Malalamiko na Rufaa kwa kuzingatia Sheria ya Ununuzi wa Umma pamoja na kanuni zake pindi wanapoona hawakutendewa haki katika zabuni walizoomba.

Katika hatua nyingine, Kessy amesema kuwa PPAA inatoa huduma ya Mkutano kwa njia ya Mtandao “Video Conference” ambapo hutumika kusikiliza mashauri ya wazabuni walioshindwa kufika moja kwa moja katika Ofisi za PPAA kwa ajili ya kusikiliza mashauri yalilowasilishwa mbele yake.

Huduma ya Mkutano kwa njia ya Mtandao imetoa fursa ya kuwasikiliza wazabuni walioshindwa kufika PPAA kutokana na sababu mbalimbali na kuiwezesha Mamlaka ya Rufani kutekeleza jukumu lake la msingi la utatuzi wa migogoro itokanayo na michakato ya ununuzi wa Umma. 

“Tangu kuanza kwa matumizi ya ‘video conference’ tayari PPAA imewasikiliza wazabuni mbalimbali kutoka katika mataifa ya Afrika Kusini, Nigeria, Poland, India na China,” amesema Kessy. 

Kadhalika, Mamlaka ya Rufani inatarajia kuunganisha Moduli ya Malalamiko na Rufaa na mfumo wa Mahakama ya Tanzania ili kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma ikiwa ni njia mojawapo ya kuimarisha matumizi ya teknolojia katika sekta ya ununuzi wa umma. 

Naye mzabuni Peter Sarungi kutoka makundi maalum alisisitiza sekta ya makundi maalum ipewe kipaumbele zaidi katika uombaji wa zabuni na kufuatilia taasisi zilizotangaza zabuni ili wapewe taarifa kama wamepata zabuni au la ili kuwawezesha kujikwamua kiuchumi ikiwemo kutumia Moduli ya PPAA. 

Matumizi rasmi ya moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST yalianza mwezi Februari, 2025.

CRDB Foundation Trains SIDO, ZEEA Officials to Strengthen MSME Support Services

0

In an effort to enhance the capacity of institutions supporting entrepreneurs in Tanzania, CRDB Bank Foundation has conducted specialised training for officials from the Small Industries Development Organization (SIDO), the Zanzibar Economic Empowerment Agency (ZEEA), and local government authorities from Mwanza, Tanga and Pemba regions.

The training is part of the implementation of the Inclusive Financial Services for Women and Youth-led MSMEs (IncluCities Project SASA), which aims to increase access to financial services and development opportunities for women and young entrepreneurs.

Opening the three-day training, CRDB Bank Head of Agribusiness Services, Shaaban Maregesi, said the programme was organised following an assessment that identified areas requiring further improvement despite the institutions having experienced staff and strong operational systems.

He mentioned key areas requiring enhancement as entrepreneurship advisory services, financial management, small and medium enterprise (SME) appraisal, customer care, and the use of digital systems in service delivery.

“There is a great opportunity to continue strengthening the capacity of these institutions so they can provide more efficient services to citizens and help them grow their businesses,” Maregesi said.

The IncluCities Project SASA is implemented through a partnership between CRDB Bank Foundation and international development organisation Enabel. So far, the project has reached more than 200 beneficiaries in Tanga, Mwanza and Pemba, while over 50 entrepreneurs have benefited from business support capital worth more than 400 million Tanzanian shillings.

Maregesi said CRDB Bank Foundation’s goal is to ensure institutions serving women and youth have greater capacity to support them in joining the formal economy, expanding their businesses and accessing financial services more easily.

“The success of women and youth entrepreneurs largely depends on the ability of institutions around them to provide quality, appropriate and timely services. This is why we continue investing in strengthening the capacity of these institutions,” he said.

Participants are expected to gain skills in six key areas, including entrepreneurship development, financial management, good governance and institutional leadership, SME appraisal, customer service, and the use of digital technologies to improve service delivery.

According to CRDB Bank Foundation, its partnership with SIDO, ZEEA, local government authorities and Enabel aims to create a better environment for entrepreneurs, increase employment opportunities and promote inclusive economic growth in Tanzania.

Beyond this project, the foundation continues to work with the government through various empowerment programmes, including the Inuka and Zanzibar Blue Economy initiatives, as well as providing loan guarantees for entrepreneurs trained through SIDO.

The training is expected to improve services offered by partner institutions, strengthen collaboration among stakeholders, and empower women and youth to effectively utilise available economic opportunities to grow businesses, create jobs and increase income.

CRDB Foundation yawezesha taasisi kukuza wajasiriamali

0

Katika jitihada za kuimarisha uwezo wa taasisi zinazowahudumia wajasiriamali nchini, CRDB Bank Foundation imeendesha mafunzo maalumu kwa maafisa wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) na watendaji wa Serikali za Mitaa kutoka mikoa ya Mwanza, Tanga na Pemba.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Inclusive Financial Services for Women and Youth-led MSMEs (IncluCities Project SASA) unaolenga kuongeza upatikanaji wa huduma za fedha na fursa za maendeleo kwa wanawake na vijana wajasiriamali.

Akifungua mafunzo hayo ya siku tatu, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wakulima wa Benki ya CRDB, Shaaban Maregesi, amesema mafunzo hayo yameandaliwa kufuatia tathmini iliyobaini kuwa, licha ya taasisi hizo kuwa na watumishi wenye uzoefu na mifumo imara ya utendaji, bado kuna maeneo yanayohitaji kuimarishwa ili kuongeza ubora wa huduma kwa wananchi.

Ametaja maeneo hayo kuwa ni ushauri wa ujasiriamali, usimamizi wa fedha, tathmini ya biashara ndogo na za kati (SME Appraisal), huduma bora kwa wateja pamoja na matumizi ya mifumo ya kidijitali.

“Kuna fursa kubwa ya kuendelea kuimarisha uwezo wa taasisi hizi ili ziweze kuwahudumia wananchi kwa ufanisi zaidi na kuwasaidia kukuza biashara zao,” amesema Maregesi.

Mradi wa IncluCities Project SASA unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya CRDB Bank Foundation na taasisi ya maendeleo ya kimataifa ya Enabel. Hadi sasa umewafikia zaidi ya wananchi 200 katika mikoa ya Tanga, Mwanza na Pemba, huku zaidi ya wajasiriamali 50 wakinufaika na mitaji wezeshi yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 400.

Maregesi amesema lengo la CRDB Bank Foundation ni kuhakikisha taasisi zinazotoa huduma kwa wanawake na vijana zinakuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kuwawezesha kuingia katika uchumi rasmi, kukuza biashara zao na kupata huduma za kifedha kwa urahisi.

“Mafanikio ya wanawake na vijana wajasiriamali yanategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa taasisi zinazowazunguka kuwapa huduma bora, sahihi na kwa wakati. Ndiyo maana tunaendelea kuwekeza katika kuzijengea uwezo taasisi hizi,” amesema.

Washiriki wa mafunzo hayo wanatarajiwa kupata ujuzi katika maeneo sita muhimu ambayo ni maendeleo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, utawala bora na uongozi wa taasisi, tathmini ya biashara ndogo na za kati, huduma kwa wateja na matumizi ya teknolojia za kidijitali katika kuboresha utoaji wa huduma.

Kwa mujibu wa CRDB Bank Foundation, ushirikiano wake na SIDO, ZEEA, Serikali za Mitaa na Enabel unalenga kujenga mazingira bora kwa wajasiriamali, kuongeza ajira na kukuza uchumi jumuishi nchini.

Mbali na mradi huo, taasisi hiyo imeendelea kushirikiana na Serikali kupitia programu mbalimbali za uwezeshaji, ikiwemo Inuka na Uchumi wa Buluu Zanzibar, pamoja na kutoa dhamana za mikopo kwa wajasiriamali wanaopata mafunzo kupitia SIDO.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuboresha huduma zinazotolewa na taasisi washirika, kuongeza ushirikiano kati yao na kuwawezesha wanawake na vijana kutumia kikamilifu fursa za kiuchumi zilizopo kwa ajili ya kukuza biashara, ajira na kipato.

Mbunge Mgonto afundisha hisabati mashuleni

0

Mbunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki, Thomas Mgonto, ameendelea na kampeni yake ya kutembelea shule za sekondari zilizopo katika jimbo lake kwa lengo la kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya sayansi, hususan Hisabati, ambayo yamekuwa yakikabiliwa na changamoto mbalimbali katika ufaulu.

Katika utekelezaji wa mpango huo ambao ameupa jina la Sikonga Mtaa kwa Mtaa na Chifu Mgonto, amekuwa akiingia moja kwa moja darasani na kufundisha somo la Hisabati kwa wanafunzi wa Kidato cha Pili na Kidato cha Nne, huku akitumia nafasi hiyo kuwahamasisha wanafunzi kujenga msingi imara katika masomo hayo muhimu kwa maendeleo yao ya kitaaluma.

Hatua hiyo ni sehemu ya jitihada zake za kutafuta namna ya kuongeza hamasa kwa wanafunzi katika kujifunza Hisabati na masomo mengine ya sayansi, ambayo yana umuhimu mkubwa katika kuwaandaa vijana kupata taaluma mbalimbali zinazohitaji ujuzi wa kisayansi na kiteknolojia.

Shule ambazo amezitembea na kufundisha wanafunzi ni shule ya sekondari Siuyu, Lighwa, Dung’unyi seminari, Ntuntu,Munghaa, Munkinya,Mkiwa,Mtaturu na Unyahati sekondari.

Mbunge huyo katika ziara zake kwenye shule hizo amekuwa akiwataka wanafunzi kuwa na nidhamu, kuhudhuria masomo kwa wakati na kutumia muda wao mwingi katika kujisomea na kufanya mazoezi ya Hisabati pamoja na masomo mengine ya sayansi.

Kunenge: Kuanzishwa kwa kongani kutafungua fursa ya ajira

0

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema eneo la Kongani Viwanda la Misugusugu, Manispaa ya Kibaha ni mradi muhimu katika kuimarisha uchumi wa Mkoa wa Pwani na kuongeza fursa za ajira kwa wananchi.

Kunenge amesema kitendo cha Manispaa ya Kibaha kutenga eneo lenye ukubwa wa hekta 350 kwa ajili ya kuanzisha Kongani Mpya ya Viwanda ni chakupongezwa hatua ambayo itasaidia kuzalisha ajira.

Pia amesema kuanzishwa kongani hiyo Manispaa imetekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo aliyaagiza.

“Na hili la mradi wa eneo la maegesho ya magari makubwa ya mizigo katika eneo la Misugusugu, ni mradi wa kimkakati utakaosaidia kuondoa changamoto ya magari makubwa kuegeshwa kando ya barabara”,amesrma Kunenge.

Amesema mradi huo wa kimkakati wa eneo la maegesho ya magari utasaidia kuongeza usalama barabarani na kutoa huduma muhimu kwa viwanda vitakavyoanzishwa ndani ya kongani hiyo.

Mkuu huyo wa mkoa amezielekeza taasisi wezeshi ikiwemo TANROADS,TARURA, TANESCO, DAWASA na TTCL, kuhakikisha zinaimarisha na kukamilisha miundombinu muhimu katika eneo hilo la kongani ya viwanda ili kuvutia wawekezaji na kuwezesha shughuli za uzalishaji kuanza mapema.

Amesema ushirikiano wa karibu kati ya Serikali, halmashauri na taasisi mbalimbali ni msingi wa kufanikisha utekelezaji wa mradi huo, ambao unatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya viwanda na uchumi wa Mkoa wa Pwani pamoja na Taifa kwa ujumla.

Awali, akitoa taarifa ya mradi Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dk. Rogers Shemwelekwa, amesema eneo hilo tayari lina huduma muhimu za maji na umeme, jambo linalolifanya kuwa kivutio kwa wawekezaji wa viwanda mbalimbali ikiwemo vya kutengeneza viatu na nguo.

Dk. Shemwelekwa amesema kupitia kongani hiyo, Manispaa inatarajia kuzalisha zaidi ya ajira 1,000, kuongeza mapato ya Serikali na Halmashauri pamoja na kuimarisha shughuli za uzalishaji na biashara katika Manispaa ya Kibaha.

Kwa upande wa mradi wa maegesho ya magari makubwa, Mkurugenzi huyo amesema huduma  imeanza kutolewa Julai mosi mwaka huu na hadi sasa magari 90 huingia na kuegeshwa kila siku katika eneo hilo. 

Mashine ya Simba yatarajiwa kung’aa dhidi ya Singida BS

0

Mashabiki wa Simba SC wanatarajiwa kushuhudia sura mpya ya timu yao katika mchezo dhidi ya Singida BS, huku kiungo mpya Ibraheem Jabaar akitajwa kuwa mmoja wa wachezaji wanaoweza kuleta tofauti kubwa ndani ya kikosi cha Kocha Steven Barker.

Jabaar anaelezwa kuwa ni mchezaji mwenye uwezo wa kucheza nafasi zaidi ya moja, ikiwemo kiungo mkabaji, kiungo mshambuliaji na winga. Uwezo wake wa kutumia vizuri mguu wa kushoto unatajwa kuwa miongoni mwa sifa zilizomshawishi Barker kumpendekeza kujiunga na Wekundu wa Msimbazi.

Ndani ya kambi ya Simba, kuna matumaini makubwa kwamba mchezaji huyo ataongeza ubunifu, kasi na ushindani katika eneo la kiungo, huku akitarajiwa kuwa miongoni mwa silaha muhimu za timu katika msimu mpya.

UCHAMBUZI

Iwapo Jabaar ataendana haraka na mfumo wa Steven Barker, Simba inaweza kunufaika kwa kuwa na mchezaji mwenye uwezo wa kubadilika kulingana na mahitaji ya mchezo. Wachezaji wa aina hii huwapa makocha chaguo nyingi za kiufundi, hasa katika mechi zinazohitaji mabadiliko ya haraka ya mfumo.

Hata hivyo, mafanikio yake yataamuliwa na kile atakachokionyesha uwanjani. Mechi dhidi ya Singida BS inaweza kuwa fursa ya kwanza kwa mashabiki kuona ikiwa sifa zinazozungumzwa kuhusu Jabaar zinaendana na kiwango chake halisi ndani ya kikosi cha Simba.

Kumbuka: Maelezo kwamba Jabaar ni “silaha ya siri” ya Barker na kwamba “Simba ina silaha za hatari kuliko kawaida” ni maoni na matarajio yanayozunguka timu, si taarifa zilizothibitishwa rasmi. Habari hii imehaririwa kwa kuzingatia mtindo wa habari za michezo huku ikitenganisha taarifa na tathmini.

Mbegu akaribia kutimiza ndoto za Ulaya baada ya Simba kutoa baraka atimkie Slavia Praha

0

Beki chipukizi wa Simba SC na timu ya taifa ya vijana ya Tanzania (Serengeti Boys), Hussein Mbegu, amepiga hatua muhimu kuelekea kutimiza ndoto zake za kucheza soka barani Ulaya baada ya klabu yake kuridhia ombi la miamba ya Czech Republic, Slavia Praha, la kumualika kwa majaribio.

Simba SC tayari imejibu rasmi barua pepe kutoka Slavia Praha na kutoa kibali kwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 17 kusafiri kwenda Czech Republic kwa ajili ya majaribio ya siku 16. Mbegu anatarajiwa kuondoka kati ya Agosti 20 na mwanzoni mwa Septemba mara tu taratibu za visa zitakapokamilika.

Uongozi wa Simba unaamini beki huyo mwenye kipaji kikubwa ataonyesha kiwango kitakachowavutia viongozi wa Slavia Praha na kufungua ukurasa mpya wa maisha yake ya soka katika moja ya klabu zenye historia kubwa nchini Czech.

Kwa sasa Mbegu yupo kambini na Serengeti Boys, inayojiandaa kushiriki fainali za Kombe la Dunia kwa vijana chini ya miaka 17. Ataruhusiwa kuondoka kwa muda kwenda kufanya majaribio hayo kabla ya kurejea nchini kuendelea na maandalizi ya michuano hiyo muhimu.

Hata hivyo, kutokana na kanuni za FIFA zinazowazuia wachezaji walio chini ya miaka 18 kusaini mikataba ya kitaalamu ya moja kwa moja, mpango uliowekwa ni Mbegu kuwa akisafiri kwenda Czech kila baada ya miezi mitatu kwa ajili ya mafunzo, kuendelea kukuzwa na kuzoea mazingira hadi atakapofikisha miaka 18 ndipo aweze kusaini mkataba wa kitaalamu.

UCHAMBUZI

Hatua hii ni ishara kwamba soka la vijana Tanzania linaendelea kuvutia macho ya klabu kubwa za Ulaya. Slavia Praha imejijengea sifa ya kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji wachanga kabla ya kuwauza katika ligi kubwa barani humo.

Kwa Mbegu, majaribio haya ni zaidi ya safari ya kawaida; ni mtihani wa kuthibitisha uwezo wake mbele ya moja ya akademi bora za maendeleo ya vijana Ulaya. Endapo atafanya vizuri, atajiweka katika nafasi nzuri ya kuwa miongoni mwa wachezaji wachache wa Tanzania kupata njia ya moja kwa moja kuelekea soka la kulipwa barani Ulaya.

Kwa upande wa Simba SC, mafanikio ya Mbegu yatakuwa ushahidi wa ubora wa mfumo wao wa kukuza vipaji na yanaweza kuongeza thamani ya klabu katika soko la kimataifa. Aidha, Serengeti Boys nayo itanufaika kwa kuwa na mchezaji anayepata uzoefu wa kimataifa kabla ya kushiriki Kombe la Dunia.

Kwa rekodi, Slavia Praha ni moja ya klabu kongwe na zenye mafanikio makubwa nchini Czech. Kikosi chake kilikuwa na wastani wa umri wa miaka 25.1 msimu uliopita, jambo linaloonyesha sera ya kuwapa nafasi wachezaji vijana. Klabu hiyo pia ilimaliza katika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu ya Czech, ikimaliza nyuma ya mahasimu wao Sparta Prague.

Iwapo Mbegu atatumia vyema nafasi hii, safari yake inaweza kuwa mwanzo wa kizazi kipya cha wachezaji wa Tanzania wanaopenya katika soka la juu barani Ulaya.

CRDB Group posts 417bn/- after-tax profit in H1, 2026

0

CRDB Group Plc has closed the first half of the year on a high note, posting a 20.3 percent jump in after-tax profit to 417bn/-, driven by stronger business volumes, growing customer activity and disciplined strategy execution.

This has enabled the leading bank, in terms of profitability and total assets, to strengthening its capacity to finance economic development, support entrepreneurship and create long-term value for customers, shareholders and the communities it serves.

Unaudited financial statements for the second quarter ending June show total Assets rose by 34 percent to 26.4trn/-, customer deposits increased by 37 percent to 18.8trn/-, while net loans expanded by 38 percent to 16.9trn/-, demonstrating the Group’s growing capacity to mobilize capital and finance productive sectors of the economy.

The results underscore the Group’s expanding role in financing businesses and entrepreneurs across agriculture, manufacturing, trade and infrastructure while deepening financial inclusion in Tanzania, Burundi and the DRC.

The Bank’s Group CEO & Managing Director, Dr. Abdulmajid Nsekela, said the strong performance reflects the successful execution of the Group’s strategy, continued investment in digital innovation and growing customer confidence across all its markets.

“Our performance reflects balanced and diversified growth across the business. Interest Income increased by more than 30 percent to 1.18trn/-, while Non-Interest Income rose to 401bn/-, driven by higher transaction volumes, continued growth in fees and commissions, and increasing adoption of our digital banking solutions. Together with strong growth in deposits and lending, these performance drivers demonstrate the resilience of our business model and our ability to consistently create value for customers, shareholders and the economies we serve.”

Dr. Nsekela noted that the Group continues to strengthen its regional footprint through its operations in Tanzania, Burundi and the Democratic Republic of Congo, complemented by CRDB Insurance, the CRDB Foundation and its Representative Office in the United Arab Emirates.

He also added that continued investment in digital banking platforms, payment solutions and customer-centric innovations is accelerating financial inclusion, improving customer experience and enabling millions of customers to access banking services more conveniently, securely and efficiently.

“As our balance sheet expands, so does our capacity to finance businesses, empower entrepreneurs, support farmers, facilitate trade and invest in innovations that improve people’s lives. Every deposit entrusted to us strengthens our ability to lend, and every loan extended creates opportunities that transform lives and economies. That remains the true measure of our success,” Dr Nsekela said.

The Bank’s Chairperson of the Board Prof. Neema Mori, said the results reflect the Board’s commitment to building an institution that creates sustainable value through sound governance, prudent oversight and disciplined execution of the Group’s long-term strategy.

“Our results demonstrate the quality of the Group’s earnings as much as their scale. Strong balance sheet growth, prudent risk management and disciplined cost optimization have enabled us to deliver sustainable profitability while maintaining a resilient capital and liquidity position. This provides a solid foundation to continue investing in innovation, customer experience and regional expansion, while consistently delivering value to our shareholders.”

Prof. Mori added that the Group’s continued growth reflects increasing confidence from customers, investors and development partners, positioning CRDB as one of Africa’s leading financial services groups with a clear purpose of supporting inclusive and sustainable economic development.

On his part the Group Chief Financial Officer, Fredrick Nshekanabo, said the results reflect not only strong growth but also the quality and sustainability of the Group’s earnings.

“Our financial performance is underpinned by disciplined balance sheet management, prudent risk practices and continued operational efficiency. We have delivered strong growth while maintaining a healthy risk profile, robust capital position and sustainable profitability. This gives us the financial strength to continue investing in innovation, customer experience and regional expansion while consistently delivering value to our shareholders.”

Nshekanabo noted that the Group maintained a Return on Equity of 29.1 percent, reflecting its ability to generate strong returns from shareholders’ capital, while the Cost-to-Income Ratio improved to 43.2 percent, demonstrating continued operational efficiency and disciplined cost management.

At the same time, the Group maintained a Non-Performing Loan ratio of 2.3 percent, underscoring prudent credit underwriting and effective portfolio management even as lending expanded significantly.

These results demonstrate that Bank’s continues to grow responsibly, expanding its lending portfolio while preserving asset quality, improving operational efficiency and maintaining one of the strongest financial positions in the market.

As the Bank enters the second half of 2026, Dr. Nsekela noted that the Group remains focused on accelerating digital transformation, deepening financial inclusion, expanding regional opportunities and supporting the productive sectors that drive economic growth.

Maasai Leader Urges Sustainable Ngorongoro Balance

0


By our Special Respondent in Busan, Korea

The 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee concluded in BEXCO, Busan, Republic of Korea, on July 29, 2026. The historic 10-day meeting approved 28 total property actions, adding 25 new sites to the World Heritage List and bringing total World Heritage properties to 1,273. Delegates from 196 States Parties to the World Heritage Convention of the United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (UNESCO) and UNESCO’s advisory bodies ICOMOS and IUCN are attending the 48th session of the UNESCO World Heritage Committee (WHC).

 Approximately 3,000 delegates, including the Director-General of UNESCO, representatives from Member States, Ministerial-level officials and Deputy Ministers from 21 member states that constitutes the World Heritage Committee attended the session.

 The Permanent Mission of Tanzania to UNESCO in collaboration with the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania organized a side event to brief UNESCO Member States from around the world on the findings of the two Presidential Commissions that conducted an assessment of land issues and voluntary relocation from the Ngorongoro Conservation Area.

 The reporter also received further clarification from Prof. Hamisi Malebo, Executive Secretary of the UNESCO National Commission of the United Republic of Tanzania, that the side event is an effort by the Government to respond to calls that have been made by various United Nations Experts, UNESCO advisory bodies and organizations requesting the Government to publish the results and full report of the Presidential Commissions that conducted an assessment of land issues and voluntary relocation from the Ngorongoro Conservation Area.

 Contributing to the discussion during the Ngorongoro Side Event at the 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee, Mr. Isack Lekisongo Meijo, a Maasai Traditional Leader from Tanzania, underscored the historic relationship between the Maasai people, livestock and wildlife within the Ngorongoro Conservation Area (NCA). Mr. Meijo emphasized that traditional Maasai pastoralism has, for generations, coexisted with wildlife though with difficulties attributable to human wildlife interactions, but have contributed to the conservation of the Ngorongoro ecosystem. 

He said, “there is no Ngorongoro without the Maasai pastoralists, and there is no Ngorongoro without the wildlife.” Using a powerful metaphor to illustrate the challenge of balancing conservation and human development, he stated: “Ngorongoro is like an aircraft carrying pastoralists, livestock and wildlife. Today, the aircraft is fully loaded, indeed overloaded. If it attempts to take off carrying more than its safe capacity, it risks crashing. For a safe and sustainable journey, it must offload its excess luggage in a carefully planned and balanced manner.”

Mr. Meijo explained that the metaphor reflects the growing pressures on the finite ecosystem of the Ngorongoro Conservation Area, where increasing human populations, human settlements, livestock and wildlife coexist within the same landscape which is not expanding under the Multiple Land Use Model (MLUM). He observed that the international discussion on achieving an appropriate balance between conservation and sustainable human development has generated differing perspectives. 

One school of thought advocates reducing pressure on the ecosystem through the voluntary relocation of pastoralist households and their livestock to areas with expanded social and economic opportunities. Another perspective argues for relocating wildlife to other areas beyond the Conservation Area to reduce ecological pressure. The MLUM in the NCA faces severe sustainability strains as growing human populations, livestock, and wildlife share a fixed land size which at the moment it has taken a collapsing gravity, and this is a wake-up call to rescue Ngorongoro. 

Mr. Meijo stressed that, regardless of differing views, the common objective is to safeguard the Outstanding Universal Value of the Ngorongoro Conservation Area while ensuring sustainable livelihoods for present and future generations of the Maasai community. He concluded by reaffirming the commitment of the Maasai community to continue working with the Government of Tanzania, UNESCO, IUCN, ICOMOS and all stakeholders to ensure that Ngorongoro remains a globally significant World Heritage Site where conservation, culture and sustainable development reinforce one another.

Following immediately after Mr. Meijo’s call, a delegate from Zimbabwe questioned and wanted to know at the operation level between the two, which option carries more risks between the relocation of pastoralists and their livestock or relocating wildlife from Ngorongoro Conservation area to reduce ecological pressure? Responding to the question on behalf of the Government of the United Republic of Tanzania, Prof. Hamisi Malebo, the Executive Secretary of the UNESCO National Commission of Tanzania, told the meeting that the easiest option is to educate and request for voluntary relocation and that can only be done with humans.

Prof. Malebo told the meeting further that, relocating wild animals is far more complex and dangerous than moving human populations, involving immense logistical hurdles, severe financial costs, and the permanent disruption of ancient, finely-tuned natural phenomena, the seasonal movement of over 1.5 million wildebeest. He reiterated the position of the Government of the United Republic of Tanzania which on the same reasons is relocating Maasai pastoralists outside of the Ngorongoro Conservation Area. 

Delegates and representatives from 36 countries expressed gratitude to the Government of the United Republic of Tanzania for hosting an informative side event on the Ngorongoro Conservation Area during the 48th Session of the UNESCO World Heritage Committee in Busan, South Korea. Contributions from the majority of the delegates conceded that, maintaining balance in the Ngorongoro Conservation Area is complex due to soaring human populations, wide spreading human settlements, rising livestock numbers, and shrinking wildlife grazing space and corridor. 

The mixed land-use model is unsustainable due to severe pressure from overgrazing, human-wildlife conflicts, and climate change. The event brought together Permanent Delegates to UNESCO, International Ambassadors, Members of the World Heritage Committee, Maasai Traditional Leaders, Conservation Experts, The Pastoralists Indigenous Non-Governmental Organizations Forum (PINGOs Forum), the Maasai International Solidarity Alliance (MISA) and other stakeholders to discuss the future of the Ngorongoro Conservation Area.

On his opening remarks Ambassador His Excellence Saidi Yakubu, The Permanent Representative of Tanzania to UNESCO and Ambassador of Tanzania to France, stressed that sustainable conservation requires openness, honest talks, and teamwork. The session highlighted collaborative efforts with UNESCO and the IUCN to align ecological preservation with the welfare of local communities. 

PPAA yashiriki kongamano la 10 la ununuzi, yawaita wadau kupata elimu matumizi ya moduli

0

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeshiriki Kongamano la 10 la Ununuzi wa Umma mwaka 2026 linaloendelea jijini Arusha, limewakutanisha wadau wa ununuzi pamoja na viongozi wa Serikali kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati ya kuimarisha Sekta ya ununuzi na ugavi nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa PPAA, James Sando, Mkuu wa Sehemu ya Huduma za Sheria PPAA, Agnes Sayi amewahimiza wadau wa ununuzi wa umma kutembelea banda la Mamlaka ya Rufani kupata uelewa juu ya majukumu na huduma mbalimbali zinazotolewa na taasisi hiyo hususan matumizi ya Moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa katika mfumo wa NeST.

PPAA imeshiriki maonesho yanayofanyika pembezoni mwa Kongamano hilo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na mchakato wa ununuzi wa umma, uamuzi juu ya rufaa zinazotokana na kufungiwa kushiriki katika michakato ya ununuzi wa umma pamoja na uamuzi juu ya malalamiko yanayotokana na kushindwa kwa Afisa Masuuli kutoa uamuzi ndani ya muda uliowekwa.

Awali, akifungua Kongamano hilo kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dk. Toba Nguvila amesema sekta ya ununuzi wa umma inahusisha sehemu kubwa ya matumizi ya fedha za serikali, hivyo kuna ulazima wa kuhakikisha fedha zote zinazotengwa zinasimamiwa kwa umakini mkubwa ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

Dk. Nguvila amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuimarisha matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika mfumo wa ununuzi wa umma ili kuongeza uwazi, kupunguza gharama za ununuzi, kuharakisha mchakato na kurahisisha ufuatiliaji wa matumizi ya fedha za umma.

“Ununuzi wa umma na ugavi ni nyenzo ya kisera na kimkakati ya Serikali katika kuchochea uzalishaji, ukuaji wa viwanda, kuongeza ajira, kuimarisha kampuni za ndani, kukuza ubunifu, na kuhakikisha maendeleo yanayopatikana yanawanufaisha Watanzania wengi zaidi,” amesema Dk. Nguvila.

Kongamano hilo la siku tatu limeanza tarehe 29 – 31 Julai, 2026 limewakutanisha wadau wa ununuzi zaidi ya 1,500. Aidha, limewakutanisha Wakuu wa Taasisi, Maafisa Masuuli, Maafisa Ununuzi, Idara Tumizi, Maafisa Sheria, Wazabuni na Taasisi binafsi.