Home Blog

Mganga wa tiba asili akamatwa kwa tuhuma za mauaji Kibaha

0

Na Mwandishi Wetu, Pwani

Jeshi la Polisi mkoa wa Pwani linamshikilia Ally Shabani (29), mganga wa tiba asili na mkazi wa Makazi Mapya, Mlandizi wilayani Kibaha, kwa tuhuma za mauaji ya Juma Nyambihira.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Muhudhwari Msuya, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), alisema tukio hilo lilifichuka baada ya ndugu wa marehemu kutoa taarifa ya kupotea kwake tangu Agosti 17. Taarifa hizo zilikabidhiwa Kituo cha Polisi Mlandizi mnamo Agosti 29, mwaka huu.

Kwa mujibu wa ACP Msuya, baada ya taarifa hizo polisi walifungua jalada la uchunguzi na kuanza kufuatilia. Hatua hiyo ilimfikisha mikononi mwao mtuhumiwa Shabani, ambaye inadaiwa alikuwa akiishi na marehemu Juma akimpatia matibabu ya asili kutokana na tatizo la uoni hafifu.

Mwili Wapatikana Katika Shimo

Kamanda Msuya alieleza kuwa mnamo Septemba 3, wakati upelelezi ukiendelea, askari walifika nyumbani alipokuwa akiishi mtuhumiwa pamoja na marehemu kwa ajili ya upekuzi. Katika eneo hilo, walibaini uwepo wa tanuri la mkaa lililokuwa karibu na nyumba hiyo, ambapo kando yake kulionekana dalili za shimo.

“Baada ya kufukuliwa, tulibaini ndani ya shimo hilo ulikuwa mwili wa marehemu Juma Nyambihira,” alisema ACP Msuya.

Mwili wa marehemu unatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu kwa taratibu za mazishi.

Mtuhumiwa Kufikishwa Mahakamani

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa mtuhumiwa Ally Shabani atafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika, huku likiendelea na hatua za uchunguzi ili kubaini undani wa tukio hilo.

Bunge: Tunawashukuru PSSSF kwa elimu

0

Watumishi wa idara ya Kamati za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wameridhishwa na huduma zinatolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa watumishi wa Umma (PSSSF) na wameshauri PSSSF izidishe ubunifu ili kurahisisha huduma kwa Wanachama wake.

Kauli hiyo imetolewa Julai 31, 2026 mjini Morogoro katika semina iliyoendeshwa na PSSSF maalum kwa Watumishi wa Bunge ambayo iliwashirikisha Makatibu wote wa kamati za Bunge. Semina ilikuwa ya kuwajengea uwelewa wa Kinga ya Jamii, hususani PSSSF.

“Hongereni sana matumizi ya mtandao hivi sasa mambo mmeyarahisisha sana, kwani kila kitu kinaanzwa na kumalizwa kwenye simu au kifaa kingine chochote cha kidijitali” alisema Angelina Sanga.

Aidha, wajumbe wa semina hiyo walishauri sera ya Kinga ya Jamii ipitiwe ili iweze kwenda na wakati.

Katika semina hiyo Mtumishi Mstasaafu wa Bunge Gerald Magili alithibitisha kuwa PSSSF ‘inalipa jana’ kwa kusema, “Nilitoa taarifa ya kuomba kibali cha kustaafu kwa mwajiri miezi sita kabla ya kusataafu, tarehe yangu ya kustaafu ilikuwa ni Juni 25, 2026, siku hiyo hiyo nilipokea mafao yangu ya kustaafu, hakika PSSSF mpo vizuri”.

Akizungumza wakati wa kufunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Hajji Moshi alishukuru ofisi ya Bunge kwa kutoa nafasi ya kufanyika semina hiyo na kusema kuwa Mfuko uko tayari wakati wowote kutoa elimu ya Kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Bunge na Wanachama wengine.



“Kwa niaba ya Menejimenti ya PSSSF, tunashukuru kupokea maoni kutoka kwenu, yote tumeyachukua na tutayafanyia kazi na yale ya Kisera tutayafikisha kwa Mamlaka husika, asanteni sana” alisema Hajji Moshi.

Kwa upande wake, Michael Chikokoto, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Kamatii za Bunge, alisema, “Tunawashukuru PSSSF kwa kuitikia wito wetu, naamini tumejifunza mengi na tatakuwa mabalozi wenu kwa watumishi wengine wa Bunge.

TZS2.6bn Project to Boost Electric Mobility Businesses in Dar

0

NMB Foundation and Mercy Corps Tanzania have signed an agreement to implement the Evolve Project, a TZS 2.6 billion initiative that will run for two years and seek to promote businesses linked to electric mobility in Dar es Salaam.

Funded by the European Union through Enabel, the project aims to empower women, young people and E-Mobility entrepreneurs through business training, technical advisory services, as well as access to grants and loans.

NMB Foundation General Manager Nelson Karumuna said the first phase of the project will benefit more than 25 businesses, while Mercy Corps will lead the implementation of various activities aimed at supporting innovators and entrepreneurs operating in the sector.

Project partners believe the collaboration will contribute to the growth of the E-Mobility sector, create employment opportunities and accelerate the adoption of clean transport technologies in Tanzania, in line with the National Development Vision 2050.

NMB Foundation, Mercy Corps wasaini mradi wa  bilioni 2.6/- kukuza biashara za E-Mobility

0

Taasisi ya NMB Foundation na Mercy Corps Tanzania zimesaini makubaliano ya utekelezaji wa mradi wa Evolve wenye thamani ya Shilingi bilioni 2.6 utakaotekelezwa kwa miaka miwili ili kukuza biashara zinazohusiana na usafiri wa vyombo vya moto vinavyotumia umeme jijini Dar es Salaam.

Mradi huo unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya kupitia Enabel unalenga kuwawezesha wanawake, vijana na wafanyabiashara wa E-Mobility kupitia mafunzo ya biashara, ushauri wa kitaalamu pamoja na upatikanaji wa ruzuku na mikopo.

Meneja Mkuu wa NMB Foundation, Nelson Karumuna, alisema awamu ya kwanza itanufaisha zaidi ya biashara 25 huku Mercy Corps ikiongoza utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kuwawezesha wabunifu na wafanyabiashara waliopo katika sekta hiyo.

Washirika wa mradi wanaamini ushirikiano huo utachangia ukuaji wa sekta ya E-Mobility, kuongeza ajira na kuharakisha matumizi ya teknolojia za usafiri safi nchini sambamba na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Bayport Marks 20th Anniversary with ICT Support for Kibamba Schools

0

Bayport Financial Services Tanzania has commemorated its 20th anniversary by donating 20 HP computers and two all-in-one printers worth TZS 100 million to the Education Department of Kibamba Constituency, reaffirming its commitment to supporting education and national development. 

The donation was officially handed over during a ceremony at Anazaki primary school Kimara, attended by the Guest of Honour, Hon. Angellah Jasmine Kairuki, Member of Parliament for Kibamba Constituency, alongside district leaders, education officials, members of the media, and Bayport representatives. 

Speaking during the handover ceremony, Bayport Financial Services Tanzania Chief Credit Officer, Amina Amani, said the donation was part of the company’s efforts to create a lasting legacy as it celebrates two decades of serving Tanzanians. 

“As we reflected on how best to celebrate this milestone, we asked ourselves how we could create a legacy that would continue making a difference long after the celebrations are over. The answer was clear, we wanted to make an investment that would continue creating value for communities and support Tanzania’s development journey,” said Amani. 

Over the past 20 years, Bayport has served more than 430,439 Tanzanians, primarily civil servants, and has disbursed over TZS 529 billion in loans, helping customers achieve their personal and financial goals. 

The donated computers and printers are expected to strengthen digital education management systems within Kibamba Constituency by improving administrative efficiency, record management, and access to technology for education officials. 

“These computers represent more than technology; they represent opportunity. They will support education officers and teachers who are shaping the future of our nation while strengthening service delivery through digital transformation,” Amani added. 

Bayport noted that as Tanzania continues to advance its digital transformation agenda, access to modern technology remains critical for enhancing public services and preparing future generations for success in a digital economy. 

The company emphasized that the donation reflects its broader commitment to being a responsible corporate citizen and an active partner in national development beyond providing financial services. 

Bayport also expressed appreciation to its customers, particularly Tanzania’s civil servants, whose trust and support have enabled the company’s growth and success over the past two decades. 

The donation forms part of Bayport’s 20th Anniversary Corporate Social Investment initiative, aimed at creating sustainable impact within the communities it serves. 

Speaking immediately after receiving the ICT equipment, the Minister of Communication and Information Technology, Angellah Jasmine Kairuki—who is also the Member of Parliament for Kibamba—said that the donation marks the official launch of the “Make Kibamba Digital” strategy, beginning with the enhancement of technology use in the education sector.

 She added that the ICT equipment’s have come at the right time, as it will facilitate education administration, inter-departmental communication, examination coordination, and service delivery to teachers, parents, and students.

 “We will begin with the education departments, but this is part of a broader plan to transform Kibamba into a digital constituency. We will continue to supply ICT equipment to secondary schools, ward offices, and other public service areas in phases,” said Kairuki.

 She noted that preparations are already complete to equip secondary schools with ICT tools—including computers, projectors, and other modern equipment—emphasizing that this rollout will take place gradually over a period of three to four years.

 Furthermore, she expressed her gratitude to Bayport Financial and the Ubungo Municipal Education Department for their cooperation, noting that Bayport will continue to collaborate with the government and the community to implement projects that benefit the public.

Mkurugenzi Bangu: Ajira 31,875 zimezalishwa kupitia WRS

0

Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRS) umezalisha ajira 31,875 katika mwaka wa fedha 2025/26 kupitia shughuli mbalimbali za mnyororo wa thamani wa mazao na bidhaa.

Hayo yameelezwa leo jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) Asangye Bangu katika mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na Idara ya Habari – MAELEZO wa kutangaza utekelezaji wa shughuli za kwa mwaka wa fedha 2025/26 na mwelekeo wa mwaka 2026/27.

Bangu, amesema ajira hizo zimetokana na shughuli za ukusanyaji wa mazao na bidhaa, uhifadhi ghalani, upimaji wa ubora, usafirishaji, upakiaji na upakuaji pamoja na huduma nyingine zinazohusiana na biashara kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala.

Aidha, amesema mchango wa WRRB katika kuongeza mapato ya Serikali umeendelea kuimarika, ambapo fedha zilizorejeshwa katika Mfuko Mkuu wa Serikali zimeongezeka kutoka Sh. milioni 22 mwaka wa fedha 2023/24 hadi kufikia Sh. milioni 140 mwaka 2025/26.

Akizungumzia kuhusu ukaguzi wa bidhaa, Bangu amesema katika mwaka wa fedha 2025/26, magunia 19,041,651 yenye uzito wa zaidi ya kilo bilioni 1.114 yalikaguliwa katika ghala mbalimbali nchini, hatua iliyochangia kuimarisha uaminifu wa mfumo na kulinda maslahi ya wadau wote wa biashara.

WRRB yaja na mikakati mitano ya kukuza mfumo wa stakabadhi za ghala

0

Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imetangaza maeneo matano ya kimkakati itakayoyatekeleza katika kipindi cha miaka mitano ijayo kuanzia mwaka wa fedha 2026/27 hadi 2030/31, yenye lengo la kuimarisha Mfumo wa Stakabadhi za Ghala, kupanua huduma zake na kuongeza mchango wake katika uchumi wa Taifa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB), Asangye Bangu, ameyasema hayo leo jijini Dodoma katika mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na Idara ya Habari – MAELEZO.

Amesema maeneo hayo ya kimkakati ni kupanua mfumo katika sekta mpya za uzalishaji, kuongeza matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), kuimarisha ushiriki wa taasisi za fedha, kuongeza uwekezaji katika miundombinu ya maghala na huduma za biashara, pamoja na kuendelea kutoa elimu, kuutangaza na kuukuza Mfumo wa Stakabadhi za Ghala. 

Bangu amesema katika mkakati wa kupanua mfumo, WRRB itaanza kuingiza sekta ya mifugo katika Mfumo huo kuanzia mwaka wa fedha 2026/27, ambapo mnada wa kwanza wa mifugo kupitia mfumo huo unatarajiwa kufanyika Wilaya ya Mvomero.

Aidha, amesema bidhaa nyingine zikiwemo mwani, ngozi, mazao ya bustani na bidhaa nyingine zitakazokidhi vigezo zitaendelea kujumuishwa katika mfumo huo. 

Amesema WRRB pia itaendelea kuboresha mifumo ya kidijitali ikiwemo WRS-MIS, WRMS na matumizi ya stakabadhi za kielektroniki ili kuongeza uwazi, ufanisi na kurahisisha utoaji wa huduma kwa wadau wa mfumo. 

Kadhalika, amesema Bodi itaendelea kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania, benki za biashara na taasisi nyingine za fedha ili kuongeza upatikanaji wa mikopo inayotumia stakabadhi za ghala kama dhamana. 

Pamoja na hayo, Mkurugenzi Bangu amewahamasisha wawekezaji kuwekeza katika ujenzi na uendeshaji wa maghala ya kisasa ili kuongeza uwezo wa nchi kuhifadhi bidhaa kwa usalama, kupunguza upotevu na kuongeza ushindani katika masoko ya ndani na kimataifa. 

Ameongeza kuwa utekelezaji wa mikakati hiyo utaongeza matumizi ya mifumo ya kidijitali katika biashara, kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi, kuongeza ajira, mapato ya Serikali na Halmashauri, pamoja na kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kupitia biashara yenye ushindani, uwazi na tija.

Hali ngumu kiuchumi yawasukuma vijana kutumiwa kisiasa

0

Imeelezwa kuwa hali ngumu ya kiuchumi imewasababisha vijana wengi kukumbwa na msongo wa mawazo na kujikuta wakitumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa.

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Wolfgang Pisa, kando ya Mkutano wa 21 wa Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na Kati (AMECEA), unaofanyika jijini Nairobi, Kenya.

Mhashamu Pisa amesema hali hiyo pia inawasukuma vijana wengi kukumbwa na shinikizo la kuhama nchini kutafuta fursa katika maeneo mengine, jambo alilosema ni hatari ikiwa hawatatayarishwa vizuri.

Pisa, ambaye pia ni Askofu wa Jimbo Katoliki Lindi, amesisitiza umuhimu wa kuzungumza na vijana mara kwa mara kupitia njia mbalimbali, ikiwamo mitandao ya kijamii, na kuwahamasisha kutumia mitandao hiyo kwa njia sahihi.

“Wengine ni wahanga wa mazingira kwa sababu ya uchumi, na moja ya matatizo makubwa ni mambo mawili. Kutokana na hizo changamoto, moja ni wanasiasa, wanasiasa wanaotumia vijana kufikisha malengo yao, lakini vijana kwa sababu hawana uchaguzi mkubwa katika uchumi, wakati mwingine ni aidha nijiunge au nitakufa njaa,” ameeleza Pisa.

Amesema kuna haja ya kuwaweka vijana hao karibu na kuwapa ushauri na maelekezo ili wasitumbukie katika tatizo hilo.

TRA yawanoa waajiriwa wapya kuzingatia weledi katika utendaji kazi

0

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka waajiriwa wake wapya kuzingatia weledi, nidhamu na maadili ya utumishi wa umma ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa walipakodi.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano wa TRA, Richard Kayombo, wakati akifungua mafunzo elekezi kwa waajiriwa wapya yanayofanyika katika Chuo cha Kodi, jijini Dar es Salaam.

Kayombo alisema mtumishi wa TRA anapaswa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu, kuwaheshimu walipakodi na watumishi wenzake, huku akisisitiza kuwa nidhamu ndiyo msingi wa mafanikio katika utendaji wa kazi.



Maadili, weledi, kuzingatia kanuni na taratibu za utumishi wao ni nguzo muhimu katika utendaji kazi ndani ya TRA na kutoa huduma bora kwa walipakodi na wananchi kwa ujumla, alisema.

Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea waajiriwa wapya uelewa wa majukumu yao, maadili ya utumishi na utamaduni wa kazi ndani ya Mamlaka ya Mapato Tanzania ili waanze majukumu yao kwa ufanisi.

BAVICHA yahoji matumizi ya mashtaka ya ugaidi

0

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA), Deogratias Mahinyila, ametoa wito kwa Watanzania na wadau mbalimbali kushirikiana kuhakikisha hali ya matumizi ya tuhuma za ugaidi dhidi ya wananchi inakomeshwa, akidai kuwa imekuwa ikitumiwa kuwabambikia watu kesi na kulichafua taifa.

Akizungumza leo katika ofisi za zamani za CHADEMA zilizopo Ufipa, Dar es Salaam, Mahinyila amesema kuwa utaratibu wa kuwasingizia na kuwabambikia wananchi kesi za ugaidi hauna haki na unaweza kuharibu taswira ya Tanzania ndani na nje ya nchi.

Amedai kuwa kauli zinazotolewa kuhusu uwepo wa ugaidi nchini zinazua hofu miongoni mwa wananchi na zinaweza kudhoofisha uhusiano wa Tanzania na mataifa mengine pamoja na kuathiri mazingira ya uwekezaji na utalii.

Mahinyila alisema taarifa zilizowahi kutolewa na Jeshi la Polisi zinaonyesha kuwa zaidi ya watu 130 wanakabiliwa na tuhuma za ugaidi, akisisitiza kuwa hali hiyo si jambo la kawaida kwa taifa na inapaswa kutazamwa kwa umakini.

Amehoji mantiki ya kauli zinazodai kuwa Tanzania haina ugaidi wakati kuna watu wanaoshikiliwa na kushtakiwa kwa makosa hayo, akidai kuwa baadhi ya watuhumiwa hao wanakabiliwa na mashtaka yasiyo ya kweli.

Aidha, ameeleza kuwa matumizi ya kesi za ugaidi yanaweza kuwa na athari kwa taswira ya Tanzania kimataifa, akidai pia kuwa yanaweza kuathiri maandalizi ya michuano ya AFCON kutokana na umuhimu unaowekwa na vyombo vya michezo duniani katika masuala ya haki za binadamu.

Samia begins official visit to Angola to deepen bilateral ties

0

President Samia Suluhu Hassan departed Tanzania on Friday for a two-day official working visit to Angola at the invitation of President João Lourenço, in a trip aimed at strengthening the longstanding relationship between the two countries.

During the visit, President Samia and President Lourenço will jointly inaugurate the Julius Kambarage Nyerere Referral Hospital in Luanda. The ceremony is expected to be attended by members of the late Mwalimu Julius Nyerere’s family, led by Mama Maria Nyerere, in recognition of his pivotal role in Africa’s liberation struggles.

Samia is also scheduled to hold bilateral talks with President Lourenço to discuss ways of expanding cooperation in key sectors and advancing issues of mutual interest between Tanzania and Angola.

As part of her programme, President Samia will attend a fundraising gala dinner organised by the spouses of African heads of state. The initiative seeks to raise funds for social and economic programmes that support the empowerment of women and young people across Africa.

According to a statement from the Presidency, the visit underscores the shared commitment of Tanzania and Angola to further strengthen their historic partnership, built during the struggle for the liberation of southern Africa and sustained through decades of close diplomatic cooperation.