Saturday, October 11, 2025
spot_img
HomeMichezo🥊 Mafia atamba: “Nitamtandika Mfilipino, ni zamu ya Tanzania kung’aa!”

🥊 Mafia atamba: “Nitamtandika Mfilipino, ni zamu ya Tanzania kung’aa!”

Bondia Ibrahim Mafia ameapa kumpiga Alvin Camique wa Ufilipino katika pambano la “Knock Out ya Mama” litakalofanyika leo Viwanja vya Posta Kijitonyama, Dar es Salaam.

“Nimemsoma vizuri, hana uwezo mkubwa. Nimejiandaa kumpa somo ulingoni,” alisema Mafia kwa kujiamini.

Bondia Yohana Mchanja naye atapanda ulingoni dhidi ya Aldri Portililo kutoka Venezuela, akiahidi “kutoa kazi na utu.”

Meneja wa Mafia Boxing Promotion, Anathol Wannah, alisema maandalizi yote yamekamilika na mashabiki wanatarajiwa kushuhudia burudani ya kipekee kutoka kwa mabondia wa ndani na nje.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments