Bodi ya Ligi imetaka klabu kuhakikisha viwanja vyao vinakidhi vigezo vilivyowekwa na Kamati ya Leseni za Klabu la sivyo zitahamia kwenye viwanja vingine.

Ofisa Habari wa Bodi, Karim Boimanda, alisema baadhi ya viwanja vimeonekana kuwa chini ya kiwango na hakuna timu itakayoruhusiwa kucheza kwenye uwanja usio na ubora.
Ligi Kuu msimu wa 2025/26 inaanza Septemba 17, na mechi za ufunguzi zitakuwa KMC dhidi ya Dodoma Jiji (KMC Complex) na Coastal Union dhidi ya Prisons (Mkwakwani).




