Monday, March 9, 2026
spot_img
HomeMichezoChama anukia Azam FC!

Chama anukia Azam FC!

Kiungo mshambuliaji wa Zambia, Clatous Chama, anatajwa kujiunga na Azam FC baada ya kumaliza mkataba na Yanga. Endapo atasajiliwa, ataweka historia ya kuchezea klabu zote tatu kubwa nchini—Simba, Yanga na Azam.

Habari zinasema Azam FC inalenga wachezaji wenye uzoefu wa kimataifa kwa ajili ya Kombe la Shirikisho, na Chama anaonekana kuwa chaguo bora. Usajili huu unaweza kuwa mbadala wa Feisal Salum anayehusishwa na Simba, Yanga, na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.

Wakati huo huo, nafasi ya Chama ndani ya Yanga huenda ikachukuliwa na Celestin Ecua kutoka Ivory Coast, ambaye ameonyesha kiwango bora akiwa Zoman FC, akifunga mabao 15 na kutoa pasi za mabao 12 msimu uliopita.

Yanga pia inadaiwa kuwaza kuwaacha baadhi ya wachezaji wake akiwemo Yao Kouassi, Jonas Mkude na Jonathan Ikangalombo. Ofisa Habari Ali Kamwe amesema majina ya wanaoondoka na wanaobaki yatatangazwa wiki ijayo.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments