Wednesday, December 10, 2025
spot_img
HomeHabariDk. Samia aeleza mkakati kuvuna soko la nyama nje

Dk. Samia aeleza mkakati kuvuna soko la nyama nje

Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk Samia Suluhu Hassan amesema uamuzi wa Serikali yake kutoa ruzuku ya chanjo, unalenga kuvuna soko la mifugo hai na nyama kimataifa.

Dk Samia ameyasema hayo leo, Jumamosi Oktoba 4, 2025 alipozungumza na wananchi wa Babati mkoani Manyara, katika mkutano wa kampeni za urais, uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi.

Amesema Serikali ilifanya uamuzi wa kutoa ruzuku ya chanjo itakayolinda afya ya wanyama na soko la kimataifa ambalo awali Tanzania ililipata lakini ilishindwa kupeleka bidhaa kwa sababu haikuwa kwenye rekodi za kimataifa kuhusu usalama wa wanyama wake.

“Soko lile tutapeleka au wanyama hai, au nyama au mazao mengine ya mifugo. Lakini ilikuwa tuthibitishwe kwanza kwamba Tanzania tumeingia kwenye orodha ambayo tunafuga na mifugo yetu ni salama,” amesema.

Ameahidi kuendelea kusimamia ufugaji Tanzania na kufungua zaidi fursa ili wafugaji wanufaike na masoko ya nje ya nchi.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments