Sunday, March 22, 2026
spot_img
HomeMichezoIbenge: Azam FC sasa inaanza kuimarika

Ibenge: Azam FC sasa inaanza kuimarika

Kocha Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema kikosi chake kinaendelea kuimarika licha ya kutokuwa kamili kutokana na baadhi ya wachezaji wake kushiriki mashindano ya CHAN.

Azam ilipata ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Polisi Rwanda baada ya sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Nyamirambo.

Ibenge amesema michezo ya kirafiki inayochezwa Rwanda itamsaidia kuandaa mfumo na kikosi bora kuelekea msimu mpya, huku akisisitiza malengo makubwa ya Azam ni kufika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Klabu hiyo haijawahi kutinga hatua hiyo tangu iingie Ligi Kuu mwaka 2008/09.

Kocha huyo mwenye mafanikio makubwa kimataifa aliwahi kuifikisha Al Hilal robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, kutwaa CHAN 2016 na DR Congo, na kuiwezesha RS Berkane ya Morocco kuchukua Kombe la Shirikisho mwaka 2020.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments