Monday, December 8, 2025
spot_img
HomeMichezoJunguni United kusajili wachezaji 13 wapya

Junguni United kusajili wachezaji 13 wapya


Klabu ya Junguni United ya Zanzibar imepanga kusajili wachezaji 13 kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu 2025/26, ili kuimarisha kikosi na kuepuka makosa ya msimu uliopita.

Katibu Mkuu, Suleiman Muidani Hassan, amesema wachezaji hao wataimarisha safu ya ushambuliaji, viungo na ulinzi. Usajili utahusisha wachezaji kutoka Zanzibar na Bara.

Amesisitiza kuwa maandalizi ya mapema yatawasaidia wachezaji wapya kuungana vyema na waliobaki. Huu unakuwa msimu wa pili kwa Junguni United kucheza Ligi Kuu ya Zanzibar baada ya kusalia kwa tabu msimu uliopita.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments