Klabu ya Kipanga FC kutoka Zanzibar imesema msimu huu imejipanga kurejea kwenye makali yake kwa kushindana ipasavyo na kutafuta makombe.

Afisa Habari wa timu hiyo, Jafari Idd, alisema tayari wamesajili wachezaji wapya sita na wanatarajia kuongeza wengine watano kwa mapendekezo ya kocha.
Alisema nguvu zaidi zimeelekezwa kwenye safu ya ulinzi na ushambuliaji, huku wakiendelea na michezo ya kirafiki ili kupata mwunganiko mzuri wa kikosi kabla ya kuanza ligi kuu ya Zanzibar.




