Sunday, December 7, 2025
spot_img
HomeMichezoKVZ kuboresha kikosi chao cha Netiboli

KVZ kuboresha kikosi chao cha Netiboli


Timu ya Netiboli ya KVZ imepanga kufanya maboresho makubwa ya kikosi chake kuelekea mashindano ya kimataifa, baada ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Netiboli Zanzibar kwa mara ya tano mfululizo, na pia kushinda Kombe la Muungano mwaka huu.

Ofisa Habari wa timu hiyo, Abduljalili Mohmed, amesema lengo kubwa ni kufanya vizuri katika mashindano ya Afrika Mashariki. Amesema timu hiyo imekuwa ikitawala mashindano ya ndani, hivyo sasa wanataka kuweka historia kimataifa.

KVZ pia inatarajia kusajili wachezaji wapya na kuwapa mikataba wale watakaosaidia kufikia malengo hayo ya kimataifa.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments