Mabasi 10 ya umeme yamewasili Zanzibar katika Bandari ya Malindi yakitokea nchini India.
Akizungunza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Naaso Shaban Ameir, alisema magari hayo ya abiria yataanza kufanya kazi mwanzoni mwa Machi mwaka huu.
Alisema yatafanya safari zake kutoka Buyu nje ya mji wa Zanzibar hadi Malindi Mji Mkongwe wa Zanzibar.




