Kocha wa KMC, Marcio Maximo, amesema hana kikosi cha kwanza bali ana timu yenye wachezaji wa ushindani.
Kauli hiyo aliitoa baada ya kikosi chake kumaliza hatua ya makundi ya Kombe la Kagame bila kupoteza mechi na kufuzu nusu fainali.
KMC ilitoka sare ya 1-1 na APR, mabingwa watetezi, huku Eric Mwijage akifunga bao la kusawazisha.
Maximo alisema mabadiliko ya wachezaji sita yaliyofanywa hayakuathiri kiwango, na anaamini kikosi chake kitakuwa tishio Ligi Kuu msimu ujao.




