Wednesday, December 10, 2025
spot_img
HomeHabariMgombea ubunge Kigamboni aahidi kuboresha huduma za jamii

Mgombea ubunge Kigamboni aahidi kuboresha huduma za jamii

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Haran Sanga, ameendelea na kampeni zake ambapo alikutana na wananchi wa Kata ya Vijibweni, Jijini Dar es Salaam.

Katika mkutano huo wa kampeni, Sanga amewahakikishia wakazi wa Kigamboni kuwa ataweka kipaumbele katika kushughulikia changamoto zinazowakabili ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama, huduma bora za afya pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya barabara.

Amesema endapo atapewa ridhaa ya kuwatumikia, changamoto hizo ambazo zimekuwa kero ya muda mrefu kwa wananchi wa Kigamboni zitakuwa historia, na maisha ya wananchi yataboreka kwa kiwango kikubwa.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments