Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba, ametoa onyo kali kwa baadhi ya wafanyabiashara wanaojihusisha na ulanguzi wa maeneo ya biashara bila kuyaendeleza.
Amesema tabia ya kuchukua maeneo mengi ya biashara na kuyaacha bila kufanyiwa shughuli yoyote inakwamisha ukuaji wa uchumi na kuwanyima fursa wengine wanaohitaji maeneo hayo kwa ajili ya uzalishaji.
Dkt. Nchemba amewataka wanaofanya vitendo hivyo kuacha mara moja, akisisitiza kuwa Serikali haitavumilia mienendo hiyo na itachukua hatua kali kwa watakaobainika kuendelea na tabia hiyo.








