Naibu Waziri Mambo ya Nje aipongeza REA kwa utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki; Cosato Chumi alasiri ya jana, tarehe 07 Agosti, 2025 ametembelea banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na kupongeza namna Wakala ilivyotekeleza Miradi mbalimbali vijijini.

Chumi amesema Miradi yote inayotekelezwa na Wakala (REA) imekuwa na athari chanya kwenye maendeleo ya Watu waishio vijijini.

“Nawapongeza REA kwa kazi nzuri na ufanisi katika kutekeleza Mradi wa Ujazilizi II (C) na Mradi wa Taa za Barabarani, Sisi Mafinga ni wanufaika wa Miradi ya REA.” Amekaririwa Chumi.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *