Rais Samia ‘awalilia’ 11 waliofariki ajali ya gari Handeni

SIMANZI, majonzi na vilio vimetanda kuanzia usiku wa jana Januari 13,2025, kwenye kata ya Segera, wilaya ya Handeni mkoani Tanga, kufuatia vifo vya watu 11 na majeruhi 13, kutokana na ajali ya gari.

Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ametuma salaam za rambirambi kufuatia vifo hivyo, kutoa pole na kuwatakia kupona haraka majeruhi wa ajali hiyo

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian, pamoja na kuwasilisha salaam za Rais Dk. Samia, amesema ajali hiyo imesababishwa na roli la mizigo lenye namba T 782 BTU.

Amesema, roli hilo liliacha barabara na kuelekea mahali walipokuwa watu wakiwaokoa majeruhi kutoka kwenye gari nyingine iliyotokea awali, ikilihusisha gari aina ya Tata lenye namba T 720 EJP.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *