“Kipindi cha uchaguzi pia huongeza tishio la uvunjifu wa amani. Ila tulichojifunza kwa wenzetu ni kuwa hili halitokei kwa bahati mbaya. Linatokea kwa sababu wapo wanaotafuta kutumia kipindi hicho kama mwanya wa kuvuruga amani. Na hawa wapo nje ya nchi na ndani ya nchi. Nje ya nchi ni wale wanaohisi kwamba wakituvuruga, yale wanayoyatamani kuyafanya ndani ya Tanzania tukivurugana pale watapata mwanya wa kuingia na kuja kuyafanya yale wanayoyatamani,” Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.





