Rais wa Afrika Kusini awasili Tanzania kushiriki Mkutano wa Dharura wa EAC na SADC

Waziri wa Madini,Anthony Mavunde, amempokea Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, aliyewasili nchini Tanzania kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Dharura wa Pamoja wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), unaofanyika Februari 8, 2025.

Mkutano huu unalenga kujadili na kutafuta suluhisho kuhusu hali ya ulinzi na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *