Mashabiki wa Bongo Fleva wamepagawa na vionjo vya wimbo mpya “Oh Mama Tetema”, toleo la nne, wa Rayvanny na msanii wa Morocco, Nora Fatehi.

Vipande vya video vilivyoachwa mitandaoni vimezua taharuki kutokana na mauno na uchezaji wa kipekee wa wasanii hao, huku mashabiki wakisubiri kwa hamu kuachia rasmi kwa wimbo mzima.