Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Beno Malisa amemkabidhi boti moja mpya PB.44 ya Ulinzi kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga.

Malisa amekabidhi boti hiyo, Agosti 22,2025 na kulitaka Jeshi la Polisi mkoani humo kuitumia vizuri kwenye shughuli za kuimarisha doria za ziwa nyasa lililopo wilayani Kyela ili na kutokomeza uhalifu.
“Boti hii ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura kuimarisha ulinzi ziwa Nyasa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema kupitia boti hiyo watafanya doria na kuimarisha ulinzi ndani ya ziwa hilo kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, Jeshi la Wananchi JWTZ, Uhamiaji na Mamlaka ya Mapato TRA.







