Wednesday, March 4, 2026
spot_img
HomeMichezoSerengeti Boys watazama ubingwa dhidi ya Uganda leo

Serengeti Boys watazama ubingwa dhidi ya Uganda leo

Timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys, inakutana na Uganda Cubs leo kwenye fainali ya CECAFA U-17, itakayopigwa katika Uwanja wa Hamza Nakivubo, Kampala.

Timu zote tayari zimefuzu kushiriki Fainali za AFCON U-17 zitakazofanyika Machi mwakani nchini Morocco. Serengeti Boys walitinga fainali kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Sudan Kusini, huku Uganda Cubs wakiwafunga Somalia 4-1.

Kocha wa Serengeti Boys, Agrey Morris, amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo huo muhimu, akiomba sapoti ya Watanzania. Mchezaji Saleh Ally amewahakikishia mashabiki ushindi na kuahidi kurudi na kombe.

Awali, timu hizi zilikuwa Kundi A na mechi yao ilimalizika kwa sare ya bila kufungana. Serengeti Boys wanahitaji kuonyesha nguvu zaidi mbele ya wenyeji Uganda ili kutwaa ubingwa.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments