Klabu ya Singida Black Stars imesitisha tamasha lao la kila mwaka, Singida Day, lililotakiwa kufanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kwa ajili ya burudani na utambulisho wa kikosi kipya cha msimu wa 2025/26.

Sababu kubwa ni ufinyu wa ratiba kutokana na maandalizi ya michuano ya CHAN inayofanyika Tanzania, Kenya na Uganda, pamoja na ratiba mpya ya Ligi Kuu itakayoanza Septemba 16.
Awali, klabu hiyo ilipanga kuwashangaza mashabiki kwa kuwatambulisha wachezaji wote wapya siku ya tamasha badala ya mitandaoni.




