Kiungo mshambuliaji Clatous Chama ameifungia Singida Black Stars bao lake la kwanza tangu ajiunge akitokea Yanga, katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KMC kwenye nusu fainali ya Kombe la Kagame.
Ofisa Habari wa Singida, Hussein Masanza, alisema usajili wa Chama haukuwa wa kubahatisha kwani walihitaji uzoefu na ubora wake wa kutengeneza mabao.
Bao la pili la Singida lilifungwa na Andre Koffi.
Singida sasa itacheza fainali dhidi ya Al Hilal ya Sudan, baada ya wapinzani hao kuwafunga APR ya Rwanda mabao 3-1.




