Klabu ya Tabora United imetangaza kukamilisha usajili wa kikosi kipya chenye thamani ya Sh bilioni tano, wakiamini kitawawezesha kufanya vizuri zaidi msimu ujao wa Ligi Kuu.

Ofisa Habari, Christina Mwagala, amesema usajili umekamilika kwa asilimia 100 na kikosi kipo kambini kujiandaa kwa msimu mpya.
Mashabiki wanatarajiwa kuwaona wachezaji wapya kwenye mashindano ya Fountain Gate. Tabora United ilimaliza nafasi ya tano msimu uliopita ikijikusanyia pointi 38.




