Klabu ya mpira wa miguu iliyokuwa ikijulikana kama Tabora United imeuzwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na sasa itatambulika rasmi kwa jina jipya la TRA United SC.
Mabadiliko haya pia yameambatana na uhamisho wa makazi ya klabu kutoka Tabora kuhamia Dar es Salaam. Hatua hiyo inafanya jiji la Dar es Salaam kuwa na jumla ya timu sita zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ambazo ni:

- Simba SC
- Young Africans (Yanga)
- Azam FC
- KMC
- JKT Tanzania
- TRA United SC
Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza ushindani na kuvutia zaidi mashabiki wa soka katika jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.




