Wednesday, March 4, 2026
spot_img
HomeMichezoTabora United yauzwa, yabadili jina kuwa TRA United SC

Tabora United yauzwa, yabadili jina kuwa TRA United SC

Klabu ya mpira wa miguu iliyokuwa ikijulikana kama Tabora United imeuzwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na sasa itatambulika rasmi kwa jina jipya la TRA United SC.

Mabadiliko haya pia yameambatana na uhamisho wa makazi ya klabu kutoka Tabora kuhamia Dar es Salaam. Hatua hiyo inafanya jiji la Dar es Salaam kuwa na jumla ya timu sita zinazoshiriki Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ambazo ni:

  • Simba SC
  • Young Africans (Yanga)
  • Azam FC
  • KMC
  • JKT Tanzania
  • TRA United SC

Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza ushindani na kuvutia zaidi mashabiki wa soka katika jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments