Wednesday, March 4, 2026
spot_img
HomeMichezoTanzania kushiriki Kabaddi Malaysia

Tanzania kushiriki Kabaddi Malaysia

Tanzania itashiriki mashindano ya Dunia ya Kabaddi ya ufukweni yatakayofanyika Malaysia kuanzia Septemba 23–29 mwaka huu.

Mwenyekiti wa Chama cha Kabaddi Tanzania, Abdallah Nyoni alisema timu za wanaume na wanawake zitaiwakilisha nchi na zitaingia kambini Septemba 8 jijini Dar es Salaam.

Alisema lengo ni kufanya vizuri na kuitangaza Tanzania kimataifa huku akitoa wito kwa wadau kusaidia vifaa na posho kwa wachezaji.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments