Ulega: TANROADS msilale

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ameagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha miradi ya dharura iliyo chini yake.

Waziri Ulega ametoa maagizo hayo kwenye mkutano wake na Menejimenti na Mameneja wa TANROADS wa mikoa yote nchini uliofanyika mjini Dodoma ambapo aliwaambia miradi ya dharula inapaswa kushughulikiwa kidharura.

“Fanyeni kazi kwa kasi tena usiku na mchana hususan kwenye miradi ya dharura ili kuwawezesha Watanzania kuondokana na adha ya miundombinu iliyoharibiwa”, amesema Ulega.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *