Warriors Queens yamaliza ligi bila pointi Zanzibar

Warriors Queens imemaliza Ligi Kuu ya Wanawake Zanzibar bila kushinda mchezo wowote kati ya sita waliocheza, wakipoteza mchezo wa mwisho dhidi ya Dunga Queens kwa mabao 2-1.

Kocha Yusuf Sape amesema msimu huu umekuwa funzo kwao na wanatarajia kufanya mabadiliko makubwa msimu ujao, hasa katika safu ya ushambuliaji ambayo haikufanya vizuri. Pia ametoa wito wa kuongezwa kwa idadi ya timu kwenye ligi hiyo ili iwe na ushindani zaidi.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *