Friday, December 19, 2025
spot_img
HomeMichezoWatanzania wazindua jukwaa la michezo la kidijitali

Watanzania wazindua jukwaa la michezo la kidijitali

Wabunifu wa Kitanzania wamezindua jukwaa jipya la kidijitali la Piku, lenye mfumo wa mnada wa kipekee unaompa ushindi mshiriki aliyeweka dau dogo la kipekee lisilorudiwa na mwingine.

Piku, iliyosajiliwa rasmi na kupata leseni ya Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania (GBT), inalenga kutoa zawadi mbalimbali za thamani kubwa kwa gharama ndogo.

Meneja Uendeshaji wa Biashara, Sia Malewas, amesema lengo ni kuleta ubunifu unaochangamsha akili na kuongeza msisimko wa kushinda zawadi.

Meneja wa Habari, Barnabas Mbunda, amesema washindi hupatikana kila wiki, mwezi na baada ya miezi mitatu, huku mshindi wa kwanza, Sabri Hamis kutoka Zanzibar, akijishindia vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni tano.

Mkaguzi kutoka GBT, Lucy Katamba, amesema jukwaa hilo limeendeshwa kwa uwazi na limeonesha mchango wa sekta ya michezo katika kukuza uchumi.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments