WCF yapongezwa kwa kujumuisha Wafanyakazi Wenye Mahitaji Maalumu

Watumishi hao walimueleza Kikwete namna WCF inavyowajumuisha kikamilifu katika kila hatua na matukio yote yanayohusisha wafanyakazi na kuwawezesha kwa kuwapatia vifaa wezeshi vinavyowarahisishia kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

“Nilipoanza kazi WCF, waliniuliza vifaa ninavyohitaji katika kutekeleza majukumu yangu, ambapo niliwaeleza na nilipatiwa vifaa hivyo na kwa sasa ninaendelea kutekeleza mjukumu yangu kikamilifu” Alieleza Bw. Emmanuel Mhehwa ambaye ni Afisa Matekelezo Ofisi ya WCF-Kinondoni

Waziri Kikwete aliipongeza WCF kwa jitihada za kuimarisha usawa na ujumuishaji mahali pa kazi, na kusisitiza umuhimu wa kuendelea kutoa elimu na huduma bora zaidi kwa wafanyakazi wote.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini WCF Dk. Abdulsalaam Omar, alimuhakikishia Waziri kuwa WCF itaendelea kuwajumuisha wafanyakazi wenye mahitaji maalumu na kuhakikisha kwamba mazingira yao ya kazi yanakuwa salama kama ilivyo kwa wafanyakazi wote.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *