Weasel asimulia maumivu baada ya kugongwa na mkewe

Mwanamuziki wa Uganda, Douglas Mayanja ‘Weasel’, ameeleza masaibu aliyopitia baada ya mkewe, Sandra Teta, kumgonga kwa gari mara tatu katika baa ya Shan’s, Munyonyo, kufuatia ugomvi wa kifamilia.

Tukio hilo lilisababisha miguu yake kuvunjika na kulazwa hospitalini akitarajiwa kufanyiwa upasuaji. Kupitia Instagram, Weasel amewashukuru mashabiki kwa salamu za pole na kuahidi kupona hivi karibuni.

Polisi wa Kampala wamedai Sandra alimgonga kwa makusudi kwa gari aina ya Toyota UBH 148Y.

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *