Mbunge wa Jimbo la Same, Anne Kilango Malecela, amesema Waziri Mkuu Mteule, Dk. Mwigulu Lameck Nchemba ni kiongozi wa watu anayefikiwa na kila mtu.
Amesema katika nafasi zake alizowahi kushika kuanzia Naibu Waziri wa Fedha na Waziri wa Fedha tofauti na mawaziri wengine amekuwa amsikivu anayesikiliza watu.
Anne Kilango amesema Rais Samia Suluhu Hassan, amegusa mioyo ya wengi kwa kumteua Dkt. Nchemba kuwa Waziri Mkuu msikivu.




