Mashindano ya Tatu ya Taifa ya kuogelea kwa watu wenye ulemavu yamepangwa kufanyika Oktoba 11, katika bwawa la Shule ya Sekondari Shaban Robert, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa TPSA, Ramadhan Namkoveka, alisema lengo ni kutambua vipaji na kupata timu ya taifa itakayoshiriki mashindano ya kimataifa.
Amesema wanahitaji Sh. milioni 15.6 kufanikisha mashindano hayo na usajili wa washiriki unaendelea hadi Septemba 29.




