Mlandege FC imesajili wachezaji sita wa kimataifa kutoka Nigeria, Ghana, Comoro na Ufaransa kwa ajili ya mashindano ya CAF na Cecafa.

Mmiliki wa timu hiyo, Abdulsatar Daud, alisema usajili huo ni mkakati wa kuhakikisha wanapiga hatua kubwa kimataifa, wakianza na Cecafa inayofanyika Dar es Salaam.




