Hatua ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kupiga simu moja kwa moja wakati wa Tamasha la Siku ya Yanga, imeibua shangwe kutoka kwa washabiki na wafuasi wa timu hiyo waliokuwepo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
Dkt Samia amepiga simu hiyo leo, Ijumaa Septemba 12, 2025 alipokuwa anafuatilia tamasha hilo, lililokuwa linarushwa mubashara, akiwa mkoani Kigoma katika ziara ya kampeni za urais.




