Thursday, December 11, 2025
spot_img
HomeHabariUzoefu wa Said Mwema wamrejesha kwenye Tume ya Amani

Uzoefu wa Said Mwema wamrejesha kwenye Tume ya Amani

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka amesema uamuzi wa Rais Samia Suluhu Hassan kumteua Said Mwema kuwa Mjumbe wa Tume ya Kuchunguza Uvunjifu wa Amani Oktoba 29, umetokana na uzoefu wake.

Ameutaja uzoefu huo, akisema Mwema amewahi kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania na katika kipindi chake, alisimamia marekebisho makubwa ya jeshi na kuandaa mkakato wa polisi jamii.

Amesema akiwa na wadhifa huo, aliliongoza jeshi hilo kupambana na uhalifu mbalimbali ikiwemo wa kuvuka mipaka, dawa za kulevya na ujambazi.

Sambamba na nafasi hiyo, amesema Mwema amewahi kuwa Mkuu wa Kanda Ndogo ya Interpol ya Nairobi na alikuwa Mjumbe katika Tume ya Kurekebisha Mifumo ya Haki Jinai.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments