Waziri Mkuu mteule, Dk. Mwigulu Nchemba amewaahidi Watanzania kuwa kila mwananchi akiwemo wa hali ya nchi atasikilizwa katika ofisi za umma na kwa nidhamu.
Dk Mwigulu ametoa ahadi hiyo,leo Alhamisi Novemba 13, 2025 bungeni jijini Dodoma, muda mchache baada ya kuthibitishwa na Bunge, akisisitiza kila Mtanzania nchi ni yake.
“Watanzania wote watasikilizwa kwa nidhamu ofisi, watasikilizwa kwa nidhamu katika ofisi za umma, “ amesisitiza Dk Mwigulu huku akipigwa na makofi na wabunge.




