Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani Oktoba, 2025 imesema baadhi ya wanasiasa na wanaharakati walitumia changamoto za wananchi kuwashawisha na kuwachochoea kushiriki ghasia kabla na wakati wa uchaguzi mkuu.
Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Othman Chande ameeleza hayo leo Jumatano Aprili 23, 2026 akitoa matokea ya ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29,2025 mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan, Ikulu Dar es Salaam
Tume hiyo imefafanua kuwa baadhi ya wanaharakati hao na wanasiasa walitumia kauli mbiu na matamko mbalimbali.

“Ushahidi taarifa umeonyesha baadhi ya wanaharakati na wanasiasa walitumia changamoto za wananchi zilizotokana na vyanzo mbalimbali kama fursa ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika ghasia hizo,”
“Tathimini yha Tume imebaini kulikowapo na vichocheo mahsusi vilivyohamasisha ari ya kufanya ghasia kabla na baada ya uchaguzi mkuu,” amesema Jaji Chande.
Amesema vichocheo hivyo vimewekwa katika makundi matatu likiwemo ya mitandao ya kijamii, akisema kwa mujibu wa mashahidi waliofika mbele ya Tume walieleza kuwa mitandao yao ilitumika kabla na baada ya uchauguzi mkuu kuwa mitandao yao ilitumika kwa kiwango kikubwa.
“Aidha waliibuka wabuni mada kwenye mitandao ‘content creator’ ikiwemo kuhamasisha wananchi wasishiriki uchaguzi mkuu au kuhakikisha haufanyiki,” amesema.





