Kauli mbiu za No reforms no election, tumedhamiria uchaguzi hautafanyika, Samia must go, tunataka kuikombo nchi yetu na hakuna uchaguzi katika serikali hii ni miongoni mwa kauli zilizochoche ghasia.
Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu Amani Oktoba, 2025 iliyowasilisha matokea ya uchunguzi mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan Ikulu leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Chande amesema kauli nyingine ni ‘Tutahakikisha nchi haisimami hadi Serikali iondoke’, ‘hakutakuwa na uchaguzi bila mabadiliko ya mfumo’ na Serikali hii imepoteza uhalali wa kuongoza nchi.




