HomeBiasharaTamasha la Uwekezaji lafanyika Zanzibar, Dk.Mwinyi atembelea Banda la NMB

Tamasha la Uwekezaji lafanyika Zanzibar, Dk.Mwinyi atembelea Banda la NMB

ZANZIBAR: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametembelea banda la Benki ya NMB katika Tamasha la Uwekezaji Zanzibar 2026 lililofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar.

Benki ya NMB ilikuwa miongoni mwa wadhamini wakuu wa tamasha hilo la kila mwaka lililowakutanisha viongozi wa serikali, wawekezaji, taasisi za fedha, watendaji wakuu na wadau wa sekta binafsi kujadili fursa za uwekezaji na kukuza uchumi endelevu wa Zanzibar.

Katika ziara hiyo, Rais Dkt. Mwinyi alipokelewa na Meneja wa NMB Tawi la Zanzibar, Ahmed Nassor, ambaye alimueleza kuhusu suluhisho mbalimbali za kifedha zinazotolewa na benki hiyo kwa wawekezaji, kampuni na taasisi zinazofanya shughuli zake Zanzibar.

Akizungumza katika banda hilo, Nassor amesema ushiriki wa NMB katika tamasha hilo unaonesha dhamira ya benki hiyo kuendelea kuwa mshirika wa karibu wa Serikali na sekta binafsi katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.

“Kwa NMB, Tamasha la Uwekezaji Zanzibar ni jukwaa muhimu la kuonesha suluhisho tulizonazo kwa wawekezaji, makampuni na taasisi zinazofanya kazi Zanzibar. Tupo tayari kusaidia mahitaji yao ya kifedha kupitia huduma za kibenki, malipo, makusanyo na mifumo ya kidijitali, huku tukiendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kusukuma mafanikio makubwa zaidi ya kiuchumi,” amesema Nassor.

Tamasha hilo linaendelea kuimarisha nafasi ya Zanzibar kama kitovu cha uwekezaji, likiwa jukwaa muhimu la kukuza ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi katika kufanikisha maendeleo ya kiuchumi.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments