Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, amemtembelea na kumjulia hali Mdau wa mziki na mlezi wa vipaji, Mkubwa Fella, nyumbani kwake, ambapo alimkabidhi msaada wa shilingi milioni 20.
Majaliwa pia alifanya naye mazoezi mepesi ya viungo na kupata fursa ya kufanya mazungumzo marefu kuhusu mchango mkubwa wa Mkubwa Fella katika kukuza na kuendeleza muziki wa Tanzania pamoja na masuala mbalimbali yanayohusu tasnia ya sanaa.
Aidha, Majaliwa ameahidi kuendelea kumtembelea Mkubwa Fella mara kwa mara ili kufuatilia maendeleo ya afya yake na kumpa faraja.









