Mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha MAKINI, Amer Hassan Ameir, ametoa ahadi ya kutoa shilingi 500,000 kwa kila mzanzibari iwapo atashinda uchaguzi wa urais wa Zanzibar.

Amer Hassan Ameir alitangaza ahadi hiyo katika mikutano ya kampeni akisisitiza dhamira yake ya kuinua ustawi wa wananchi na kuimarisha maendeleo ya kiuchumi visiwani humo.
Aidha, mgombea huyo ameahidi kuwekeza katika miradi itakayoongeza ajira, kukuza biashara ndogo na za kati, pamoja na kuboresha huduma za jamii. Hii ni moja ya ahadi zake zinazolenga kuleta mabadiliko chanya na kufanikisha ustawi wa wananchi wa Zanzibar.




