Wednesday, December 10, 2025
spot_img
HomeBiasharaDkt Samia: Tutajenga soko la kisasa Mwanga

Dkt Samia: Tutajenga soko la kisasa Mwanga

Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amesema Serikali yake katika miaka mitano ijayo, itajenga soko la kisasa wilayani Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro, ili kuwasaidia wakulima kuuza bidhaa zao.

Dkt Samia ametoa kauli hiyo leo, Jumanne Septemba 30, 2025 alipozungumza na wananchi wa Mwanga mkoani Kilimanjaro, katika mkutano wake wa kampeni za urais.

Hatua ya ujenzi wa soko hilo kwa mujibu wa Dkt Samia, inachochewa na eneo hilo kuwa na wakulima wengi wa mpunga, mahindi na maharage, lakini wamekosa soko.

Kutokana na kukosekana kwa soko, ameeleza wakulima hao hawafaidiki na shughuli zao, hivyo anacholenga ni kuhakikisha wananufaika.

“Niwaambie ndugu zangu, kwamba tunakuja kujenga soko. Soko kubwa soko la kisasa,” amesema.

Ujenzi wa mradi huo, utaambatana na soko lingine katika Kata ya Kileo, ili kuwaepusha wakulima wa eneo hilo na kuuza bidhaa zao kwa walanguzi.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments