Rais wa TFF, Wallace Karia, ametabiri msimu wenye ushindani mkubwa zaidi kwenye Ligi Kuu ya Wanawake baada ya JKT Queens kuifunga Simba Queens 2-1 na kutwaa Ngao ya Jamii.
Karia alipongeza maandalizi ya timu zote, akisema ushindani huo unaonyesha ukuaji wa soka la wanawake. Ameomba wadhamini kujitokeza kusaidia ligi hiyo ili “kutimiza ndoto ya soka la wanawake lenye heshima nchini.”




