Tuesday, May 19, 2026
spot_img
HomeHabariDk Samia: Tutashirikiana kuendeleza matumizi nishati ya nyuklia

Dk Samia: Tutashirikiana kuendeleza matumizi nishati ya nyuklia

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Tanzania ipo tayari kushirikiana na mataifa ya Afrika pamoja na taasisi za kimataifa kuendeleza matumizi ya nishati ya nyuklia ili kuimarisha usalama wa nishati na maendeleo ya muda mrefu barani Afrika.

Akizungumza katika Mkutano wa Ubunifu wa Nishati ya Nyuklia Afrika (NEISA 2026) uliofanyika Kigali nchini Rwanda Mei 19, 2026, Dkt Samia amesema mahitaji ya umeme yanaongezeka kwa kasi kutokana na ukuaji wa viwanda, miji na sekta mbalimbali za uchumi, hivyo nishati ya nyuklia ni moja ya suluhisho muhimu kwa mustakabali wa Afrika.

“Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi za Afrika, taasisi za kimataifa na sekta binafsi kuhakikisha nishati ya nyuklia inakuwa chachu ya ustawi na usalama wa nishati Afrika,” amesema Dkt Samia.

Mkutano huo uliwakutanisha viongozi wa sera, wataalamu wa nishati na wadau wa maendeleo kujadili namna ya kuharakisha matumizi ya nishati ya nyuklia kama chanzo salama na safi cha umeme kwa maendeleo ya uchumi wa Afrika.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments