Saturday, May 9, 2026
spot_img
HomeBiasharaData na Mobile Money zaongeza faida ya Airtel Africa mara mbili

Data na Mobile Money zaongeza faida ya Airtel Africa mara mbili

‎Matumizi ya huduma za intaneti na Airtel Money yameendelea kuwa nguzo kuu ya ukuaji wa mapato ya Airtel Africa, baada ya kampuni hiyo kutangaza ongezeko kubwa la mapato na faida kwa mwaka ulioishia Machi 31, 2026.

‎Faida halisi ya kampuni imeongezeka zaidi ya mara mbili hadi dola milioni 813 kutoka dola milioni 328 mwaka uliopita, huku mapato yakipanda kwa asilimia 29.5 na kufikia dola bilioni 6.42.

‎Kampuni hiyo imeeleza kuwa mafanikio hayo yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na kuongezeka kwa matumizi ya data na huduma za Airtel Money, ambazo zimeendelea kuongeza matumizi ya huduma za kidijitali kwa wateja wake katika masoko 14 barani Afrika.

‎Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Sunil Taldar, amesema matokeo hayo yanaonyesha uimara wa biashara ya kampuni pamoja na uwekezaji unaoendelea katika miundombinu ya mtandao na huduma za kidijitali.

Airtel Tanzania

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments