Sunday, March 22, 2026
spot_img
HomeBiasharaTRA yakamata bidhaa mbalimbali za magendo Bandari ya Bagamoyo

TRA yakamata bidhaa mbalimbali za magendo Bandari ya Bagamoyo

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani imekamata bidhaa mbalimbali za magendo katika Wilaya ya Bagamoyo ikiwemo viroba 50 vya mchele, madumu 10 ya mafuta ya kula na sabuni boksi 25 aina ya Malaika.

Kwa mujibu wa Meneja Msaidizi wa Forodha mkoa wa Pwani,  Melinda Matinyi bidhaa hizo za magendo zilkamatwa Machi 19.2026 kufuatia operesheni ya udhibiti wa bidhaa zinazoingizwa nchini au kusafirishwa bila kufuata taratibu za kisheria za forodha.

Alisema bidhaa zilizokamatwa zimehifadhiwa katika yadi ya TRA Bagamoyo kwa ajili ya kuendelea na taratibu za kiforodha na hatua nyingine za kisheria.

‎Mamlaka ya Mapato Tanzania imeendelea kutoa wito kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kufuata sheria na taratibu za kodi na forodha ili kuepuka hasara na adhabu zinazoweza kujitokeza pindi wanapojihusisha na vitendo hivyo.

RELATED ARTICLES

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

- Advertisment -
NMB Tanzania

Most Popular

Recent Comments